YOUTUBE PLAYLIST

Thursday, May 20, 2010

Top Ten Show


1989/90 Radio Tanzania kwa ushirikiano na Umoja wa Vijana na CHAMUDATA waliweza kuendesha mashindano makubwa ya bendi yaliyoshirikisha karibu bendi zote Tanzania. Haijawahi kutokea project kubwa namna hiyo ya muziki na vigumu kuelewa kama itawezekana tena katika mazingira ya sasa. Pichani ni Vumbi na marehemu Mbwana Cocks katika picha iliyotoka gazeti la Uhuru wakiwa katika jukwaa Vijana Kinondoni. wakati huo Cocks alikuwa ndo ametoka Vijana Jazz na kuhamia Orchestra Maquis Original, akawa anapiga second solo, rythm akisindikizwa na William Masilenge, solo akiweko Vumbiiiiiiiiiiii

Choggy Sly

Nahisi najua Choggy Sly angesema nini angekuwa hai kama angejua nimeweka picha hii hapa, God he was a great guy. Pembeni yake ni mwanamuziki kutoka South Africa Vuli, aliyefanya mengi katika muziki nchini akiwa na dada yake Nini aliyekuwa akiimbia Afro70.Vuli baadae alikuwa akipiga trumpet katika kundi la Lucky Dube

Mabrothermen get together

Pamoja na yote vijana walipenda sana kuparty, kwa kila kisingizio ilitengenezwa party kulikuwa na party every week end. Unamtambua nani hapa? Kati ya hawa ni wachangiaji wakubwa wa blog hii pengine watakumbuka walikuwa wapi siku hiyo mabitozi hawa.Katika picha 'soul brother no 1' yumo. Na MJ nae ndani hahahahahaha those were the days. Wazee Maro mnamuona? Dimando huyo wa pili toka kushoto picha ya juu, mpaka leo hataki kunenepa anataka kuvaa slimfit bado.Angalia walivyovaa!!!!

Tunawakumbuka


Panjula na Kitonsa

Wednesday, May 19, 2010

Magwiji wa kweli

Hawa wanamuziki kama unavyowaona wanapiga saxophone , walikuwa na mengi zaidi wanafanana walikuwa pia wanaweza kupiga vizuri vyombo vingine, japo hawakuwahi kuwa bendi moja lakini wote waliwahi kuwa katika bendi zilizorekodi muziki ambao unapendwa mpaka leo ni akina nani na walipiga vyombo gani na walipitia bendi gani?

Simba wa Nyika

Tanga ni mji ambao umekuwa chimbuko la mambo mengi katika ulimwengu wa muziki. Hata muziki wa dansi uliingia nchini kupitia Tanga. Kilimo cha katani chini ya mpango wake wa SILABU (Sisal Labourers Beureau) iliwezesha watu kutoka sehemu mbalimbali kukutana Tanga kwa ajili ya ajira ya kukata mkonge, na hivyo mchanganyiko huo wa makabila ulileta uchangamfu wa kimuziki katika jiji la Tanga mapema sana kuliko miji mingine. Kati ya mazao ya Tanga ni bendi maarufu ya Simba wa Nyika ambayo wanamuziki wake walitoka Tanga na kuweka makao yao kwa muda Arusha wakiitwa Arusha Jazz na mtindo wao Wanyika. Vijana hawa walipohamia Kenya wakajiita Simba wa Nyika na waliwasha moto wa nyika kimuziki na nyimbo zao tamu. Hapa ni picha yao mojawapo.

Kitendawili tena

Naleta picha nyingine ya wanamuziki wa zamani, bahati mbaya kuna mmoja katika picha hii amekwisha tangulia mbele ya haki, wa kwanza kushoto ni Salim Willis, drummer, na baadae mpiga gitaa wa Afro70, wa kwanza kulia ni mwanamuziki wa toka enzi hizo na mpaka leo bado yuko jukwaani je unamfahamu ameshiriki katika miziki mingi inayopendwa sana. Unakumbuka bendi alizopitia?

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...