Siku maalumu ya Mavokali ni leo Ijumaa pale Mawasiliano Park Ubungo, jirani kabisa na jengo yalipo Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania yaani TCRA.
Kuanzia saa mbili kamili usiku na Twanga Pepeta Kisima cha Burudani.
YOUTUBE PLAYLIST
Friday, August 12, 2022
USIKU WA MAVOKALI KILA IJUMAA NA TWANGA PEPETA
Tuesday, August 9, 2022
MWANAMUZIKI SHAABAN KIBENGO KABUMBI -CADET BONGOMAN HATUNAE TENA
Marehemu SHAABAN KIBENGO- CADET BONGOMAN |
Mwanamuziki Shaaban Kibengo Kabumbi, aliyewahi kuwa muimbaji wa bendi kadhaa nchini kama Akudo Sound, Bicco Stars, na African Revolutions. Amefariki dunia alfajiri ya leo. Shaaban alikuwa maarufu kwa jina la Cadet Bongoman, jina alilolipata enzi alipokuwa dansa miaka ya 90 kutokana na umahiri wake wa kumuiga vizuri Kanda Bongoman.
Katika miaka ya karibuni alikuwa akipiga muziki na kundi la Mambosasa Mini Band katika hoteli mbalimbali na kwa muda mrefu katika hoteli ya Concord Kariakoo.
Mazishi ya Shaaban yalitegemewa kufanyika Kimara Mwisho leo 9 Agosti 2022
Shaaban kulia akiwa na marehemu Papa Wemba katika moja ya maonyesho |
MUNGU AMLAZE PEMA SHAABAN KIBENGO
Sunday, July 31, 2022
ASANTE SANA DR KEDMOND MAPANA, KATIBU MTENDAJI MPYA WA BASATA
HAKUNA RAHA KUBWA KAMA PALE UNAPOONA SERIKALI INAZUNGUMZA NDOTO ZA WASANII, SERIKALI INAPOZUNGUZA MIPANGO YA KUENDELEZA SANAA KWA MUDA MREFU NA KWA KUTENGENEZA MFUMO UTAKAOFAIDISHA WASANII NCHI NZIMA. HAKIKA MWANGA UNAONEKANA WA KUONDOKANA NA ZILE SHUGHULI ZA KUTENGENEZA MATUKIO AMBAYO NI YA SIKU MOJA NA KWA WASANII WACHACHE MAARUFU.
Friday, July 29, 2022
TWANGA PEPETA KISIMA CHA BURUDANI KILA IJUMAA MAWASILIANO PARK
Vokali kali toka kwa Charles Baba Kingunge, akiwa na wakali wenzake wa Twanga Pepeta Sugu Kisima cha Burudani, kila Ijumaa huwa zinasikika Mawasiliano Park Ubungo jirani kabisa na jengo yalipo Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania yaani TCRA kuanzia saa mbili kamili usiku. Unakosaje?
Thursday, July 28, 2022
Subscribe to:
Posts (Atom)
SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...
-
Mara baada ya kutoa ule wimbo maarufu wa Kisambaa Shakaza, Eddy Sheggy mwenyewe na Wasambaa wengine wakaanza kuitwa Shakaza. Eddy Sheggy ali...
-
Suleiman Mbwembwe, aliyekuwa anajulikana pia kwa jina la Electronic Voice, alikuwa mwimbaji na mtunzi aliyeng'ara katika enzi zake. Aki...
-
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...