YOUTUBE PLAYLIST

Sunday, June 20, 2010

Disco

Haya djs walikuwa, na bado ni watu muhimu katika shughuli za muziki Tanzania, labda nikupe maelezo mafupi. Baada ya Biribi kupumzika, akazuka kijana huyu, kwanza kwenye parties maeneo ya Upanga, na baadae kuwa dj maarufu aliyejulikana kama Dj Emperor, akiburudisha sana pale Agip Motel na kisha kuhamia ghorofa ya saba New Africa Hotel, alifanya mambo makubwa Arusha pia wapenzi wa disco mnamkumbuka? na disko lake liliitwaje?




Friday, June 18, 2010

Tancut almasi Orchestra enzi hizo

Tancut Almasi katika onyesho mojawapo. Hawa dada wawili, ni Nana Njige(marehemu), na Nuru Mhina ambaye baadae aliolewa na Kabeya Badu ambaye ni muimbaji katika bendi ya Wazee Sugu. Trumpet Ray Mlangwa magitaa John Kitime na Kawelee Mutimwana,

Wednesday, June 16, 2010

Saba saba 2

Kama ambavyo niliwataarifu ni kweli wanamuziki wa zamani wamepania kufanya show moja ya pamoja siku ya Sabasaba katika ukumbi wa Karimjee. Pia imeonekana shughuli hii iwe inafanyika kila mwaka na ilenge kuwa tamasha la muziki la kila mwaka hapa Tanzania Bara. Wanamuziki wamekuwa wakifanya mazoezi ambayo kwa kweli yatawafurahisha wapenzi wa muziki wa Tanzania. Nawaletea picha mbalimbali za wanamuziki waliomo katika mazoezi hayo nina uhakika mtakuwa mnawafahamu wengi








Monday, May 31, 2010

SABA SABA 2





Wanamuziki kadhaa wa zamani walikutana kuongela onyesho la wanamuziki wa zamani litakalofanyika siku ya Sabasaba. Mazoezi yataanza wiki ijayo. Pichani toka juu, Muhidin gurumo, Abdul Salvador, King Kiki na Rehani Bitchuka, Kabeya Badu na Ally Jamwaka, Jeff

Thursday, May 27, 2010

Mayaula Mayoni hatunae tena

Mayaula mayoni si jina geni kwa Watanzania. Pamoja na kuwa mwanamuziki mtunzi katika lile kundi maarufu la TP OK Jazz,chini ya Franco Luambo, Mayaula aliwahi kuwa mchezaji wa Young Africans. Mayaula alikuwa msomi mzuri wa Teknolojia ya Computer. Kwa miaka mingi karibuni alikuwa akaiishi Magomeni Mikumi Dar Es Salaam, huku akifanya kazi Ubalozi wa nchi yake hapa Tanzania.
Mayaula amefariki asubuhi ya tarehe 26 May 2010 huko Brussel Ubelgiji. Alikuwa na miaka 64. Mungu amlaze peponi pema. Sikiliza tungo yake hii akiwa na TP OK Jazz.

Wednesday, May 26, 2010

Shakaza Eddy Sheggy




Mara baada ya kutoa ule wimbo maarufu wa Kisambaa Shakaza, Eddy Sheggy mwenyewe na Wasambaa wengine wakaanza kuitwa Shakaza. Eddy Sheggy alikuwa mwimbaji mzuri na mtunzi mzuri sana. Kati ya bendi alizopitia ni Super Rainbow, Vijana Jazz, Bantu Group, Washirika Stars. Picha mbili za juu ni Eddy akifanya onyesho na Super Rainbow katika uwanja wa Mnazi Mmoja, chini ni wakati akiwa Vijana Jazz

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...