YOUTUBE PLAYLIST

Tuesday, February 2, 2010

Je unajua kuwa ile ule wimbo maarufu unaoimbwa kila wakati wa birthday unalindwa na hakimiliki? Wimbo huu ni mali ya America Online ambao hupata kiasi cha dola milioni 2 kila mwaka kutokana na mirabaha ya matumizi ya wimbo huu. Na wimbo utakuwa mali yao hadi mwaka 2030


Jerry Nashon aka Dudumizi, moja ya waimbaji na watunzi mahiri waliowahi kupita katika anga la muziki Tanzania, nyimbo zake nyingi kama Imakulata (Bima Lee), Thereza, VIP (Vijana Jazz) zilimuweka katika matawi ya juu katika enzi zake

Ujaji wa vinanda aina ya synthesizer ulitoa hukumu ya kifo kwa taaluma ya vyombo vya upulizaji katika bendi nyingi Tanzania. Msondo ngoma wamebakia na msimamo ambao umeweka Bendi hiyo katika ngazi ya pekee kutokana na kubakia na wapulizaji ambao ni wazuri sana, pichani, Mnyupe na Romario katika onyesho moja mjini Tanga
Anajulikana pia kama Zungu, ni mcheza show maarufu wa African Stars Band, huyu ni mtoto wa Salim Willis ambae alikuwa mojawapo ya wanamuziki wa Afro 70 Band. Willis kwa sasa anafanya shughuli nyingine japo bado anaweza kupiga gitaa vizuri kama ilivyoonekana kwenye album ya mwisho ya Marehemu Patrick Balisidya

Hii ni label ya santuri mojawapo ya zamani. Katika miaka hii kulikuwa hakuna wizi wa kazi za sanaa kama ilivyo sasa. Teknolijia ilikuwa haiwezeshi mtu kukaa chumbani kwake na kunakili kazi za watu

Monday, February 1, 2010

Two generations

Huwa nafurahi kila nikipata chance ya kuona show ya Shaa u r great girl

Matangazo ya Bendi zamani yalikuwa yakipambwa na vituko mbalimbali. Wakati huo matangazo yalikuwa yakitoka katika magazeti tu. Na magazeti yalikuwa hayana teknolojia ya kutoa picha za rangi. Hili ni tangazo la bendi ya Maquis ambayo kwa wakati huo ilikuwa na wanamuziki karibu hamsini

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...