YOUTUBE PLAYLIST
Wednesday, May 26, 2010
SABA SABA
Ile siku ya kuvaa slimfit,jackson 5, raizon na muziki ulioendana na kipindi hicho inazidi kukaribia. Vikao vya matayarisho vinaendelea. Wanamuziki ambao watapanda jukwaani siku hiyo ni wale wa enzi zile na kupiga muziki wa enzi zao, tunategemea kusikia wakongwe hao wakiporomosha muziki kutoka sehemu mbalimbali za dunia. Pichani ni washiriki wa kikao kilichoendelea leo 26/5/2010. Waliohudhuria Waziri Ally,Ahmad Dimando, Juma Ubao,Crispin Stephan, Godfrey Mahimbo,Kanku Kelly, Jerry Tom, John Kitime.
Sunday, May 23, 2010
Patrick Pama Balisidya
Mwaka 1996 kwa ufadhili wa Ubalozi wa Netherlands lilifanyika tamasha kubwa la muziki Mnazi Moja, bendi kama Vijana Jazz, Polisi Jazz, Zaita Muzika, Maquis Original, Namtu Group, Shikamoo Jazz, zilishiriki. Hapa Patrick akishirikiana na Vijana Jazz, nyuma yake ni Fred Benjamin mwimbaji wa sauti ya kwanza Vijana Jazz, ambae naye ametangulia mbele ya haki. Siku hii alipiga wimbo wa Ni mashaka na hangaiko akishirikiana na Shikamoo Jazz
Saturday, May 22, 2010
Thursday, May 20, 2010
Top Ten Show
1989/90 Radio Tanzania kwa ushirikiano na Umoja wa Vijana na CHAMUDATA waliweza kuendesha mashindano makubwa ya bendi yaliyoshirikisha karibu bendi zote Tanzania. Haijawahi kutokea project kubwa namna hiyo ya muziki na vigumu kuelewa kama itawezekana tena katika mazingira ya sasa. Pichani ni Vumbi na marehemu Mbwana Cocks katika picha iliyotoka gazeti la Uhuru wakiwa katika jukwaa Vijana Kinondoni. wakati huo Cocks alikuwa ndo ametoka Vijana Jazz na kuhamia Orchestra Maquis Original, akawa anapiga second solo, rythm akisindikizwa na William Masilenge, solo akiweko Vumbiiiiiiiiiiii
Choggy Sly
Nahisi najua Choggy Sly angesema nini angekuwa hai kama angejua nimeweka picha hii hapa, God he was a great guy. Pembeni yake ni mwanamuziki kutoka South Africa Vuli, aliyefanya mengi katika muziki nchini akiwa na dada yake Nini aliyekuwa akiimbia Afro70.Vuli baadae alikuwa akipiga trumpet katika kundi la Lucky Dube
Mabrothermen get together
Pamoja na yote vijana walipenda sana kuparty, kwa kila kisingizio ilitengenezwa party kulikuwa na party every week end. Unamtambua nani hapa? Kati ya hawa ni wachangiaji wakubwa wa blog hii pengine watakumbuka walikuwa wapi siku hiyo mabitozi hawa.Katika picha 'soul brother no 1' yumo. Na MJ nae ndani hahahahahaha those were the days. Wazee Maro mnamuona? Dimando huyo wa pili toka kushoto picha ya juu, mpaka leo hataki kunenepa anataka kuvaa slimfit bado.Angalia walivyovaa!!!!
Subscribe to:
Posts (Atom)
SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...
-
Mara baada ya kutoa ule wimbo maarufu wa Kisambaa Shakaza, Eddy Sheggy mwenyewe na Wasambaa wengine wakaanza kuitwa Shakaza. Eddy Sheggy ali...
-
Suleiman Mbwembwe, aliyekuwa anajulikana pia kwa jina la Electronic Voice, alikuwa mwimbaji na mtunzi aliyeng'ara katika enzi zake. Aki...
-
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...