Hawa ndio The Jets (1972), ambao baadae walikuja kuwa STC Jazz, ambayo ndio chanzo cha Biashara Jazz. Waliopo hapa wa kwanza Belino, Raphael Sabuni, Mgoro katika moja ya maonyesho yao. Marijanio Rajab alijiunga na kundi hili, na kuimba wimbo kama.... Ilikuwa usiku wa manane.
YOUTUBE PLAYLIST
Tuesday, April 20, 2010
The Jets
Monday, April 19, 2010
Flaming Stars
Afro70 1974
Dar Es Salaam Jazz-majini wa bahari
Dar Jazz ndiyo kati ya bendi za kwanza nchini. Bado kuna utata wa kumbukumbu kwani katika kipindi cha mwanzo kulikuwekona Coast Social Orchestra inayosemekana ilikuja kuwa Dar Jazz. Wakati huohuo kulikuweko na YMCA Social Orchestra, hivyo ipi ya mwanzo ni kitendawili bado. Pichani ni Dar Jazz 1968. King Michael Enoch akiwa na kofia na nadhani hatupati taabu kumtambua Patrick Balisidya.Kama unavyoona amlifier ya magitaa ilikuwa moja tu, na chini kwenye kiti, kuna amlifier ambayo iliunganishwa kwenye cone spikas, zile spika za chuma tunazoziona kwenye sehemu za ibada na hizo ndizo zilikuwa kwa ajili ya waimbaji.
Tanzania All Stars
Ukitaka kujua umahiri wa wanamuziki enzi hizo ni vizuri ukazisikiliza nyimbo za Tanzania All Stars. Karibuni nitazitundika wote tuzisikilize, katika wimbo wa Samora, Zahir Ally Zoro aliimba Kireno, Jabali aliimba Kiarabu, Aziz Varda Kihindi we bwana wee. Haya tujikumbushe kwa kuwataja majina wote unaowaona hapo juu.
Usimkwae mtu likwae chua
Chakachua ndio ulikuwa mtindo wao, walikuwa na mpiga solo ambae wapiga magitaa wote waliomjua wanamheshimu kwa upigaji wake. Kuna mwanamuziki Mtanzania aliyeko Japan aliwahi kunambia kuna siku aliwahi kumsikilizisha muziki wa Chakachua mpiga gitaa mahiri George Benson, George Benson alisikitika sana kusikia aliepiga gitaa vile ameshafariki kwani alitaka wakutane watengeneza kitu cha pamoja, huyu si mwingine bali ni Michael Vicent. Na bendi ilikuwa Urafiki Jazz iliyokuwa chini ya Kiwanda cha nguo cha Urafiki Dar Es Salaam
Sunday, April 18, 2010
TP OK Jazz Dar es Salaam 1974
Mwaka 1974, TP OK Jazz chini ya Lwambo Lwanzo Makiadi walitembelea Tanzania, na kupiga show tatu. Moja National Stadium, Diamond na Bahari Beach. Onyesho la Bahari Beach walishirikiana na Afro 70. Matokeo ya ushirikiano huo yalijitokeza kwa nyimbo kadhaa zilizopigwa na Afro 70 kuwa na solo lilifuata mipigo ya Franco. Nyimbo kama Dada Rida, Umoja wa wakina Mama, ni baadhi ya nyimbo hizo,tena hii nyimbo ya pili ilikuwa kama kopi ya wimbo Georgette wa Franco. Ujio huo ulianzisha utamaduni uliodumu kwa muda mrefu wa bendi kupenda kutumia vifaa vya aina ya Ranger FBT.
Subscribe to:
Posts (Atom)
SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...
-
Mara baada ya kutoa ule wimbo maarufu wa Kisambaa Shakaza, Eddy Sheggy mwenyewe na Wasambaa wengine wakaanza kuitwa Shakaza. Eddy Sheggy ali...
-
Suleiman Mbwembwe, aliyekuwa anajulikana pia kwa jina la Electronic Voice, alikuwa mwimbaji na mtunzi aliyeng'ara katika enzi zake. Aki...
-
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...