YOUTUBE PLAYLIST

Saturday, February 6, 2010

Mzee Humplick aliwahi kupigwa marufuku

Je unajua kuwa Mzee Frank Humplick ambaye ndiye mtunzi wa nyimbo kama Chaupele Mpenzi, Embe dodo imelala mchangani, aliwahi kutunga nyimbo iliyopigwa marufuku na kusakwa nyumba hadi nyumba ili kusibakie hata nakala ya wimbo huo? Maneno ya wimbo huo yalisema hivi:
Uganda
nayo iende

Tanganyika ikichangaruka, Kenya na Nyasa zitaumana

Nasikia fununu wanavyoichanachana China, Kitisho!

I am a democrat, I don't want communism, English, Yes, No I don't know, Kizungu sikijui

Wanyika msishindane na Watanganyika

Wimbo huo ukaanza kutumika kabla ya mikutano ya Mwalimu Nyerere na kuanza kuwa maarufu kama wimbo wa kudai uhuru, wakoloni haraka sana wakaona wimbo huu utaweza kusababisha vurugu kama ambazo zilikuwa zinaendelea Kenya chini ya Maumau. Serikali ikaupiga marufuku na kuanza kuusaka nyumba hadi nyumba

Friday, February 5, 2010

Young Audiences Music Award

2 February 2010, Jeunesses Musicales International (JMI) launches a call for nominations for the Young Audiences Music Award 2010, an international prize that will celebrate top musical productions for children and youth.

"Looking at the quality of productions presented in schools and within education and audience development programs today, it's obvious that a new standard has been set" said JMI Secretary General Blasko Smilevski "What we see are productions nothing short of spectacular - in terms of artistry but also in terms of message. The once common ‘What instrument is this? lesson' is being fast replaced by subtle teachings on social, environmental, and intercultural issues through music."

Do you know a young audiences production with impact? Visit the all-new www.yama-award.com to apply today! Deadline for submissions is May 1st 2010, thereafter an international panel of experts will select 5 finalists to be presented online and open for public vote. The best productions, one selected by the expert panel and the other by public vote, will win €2,500 each, towards a future production for young people and children. The winners will be revealed at the Young Audiences Music Award ceremony to take place in Skanderborg, Denmark in October 2010.

The Young Audiences Music Award aims to identify and support cutting-edge productions that impact young people with both social and artistic value, targeting and engaging vulnerable/at-risk groups of youth from marginalized communities and deprived areas, addressing issues of vital concern (eg. violence, poverty, discrimination, abuse, HIV/AIDS) and that use music as a tool to promote intercultural dialogue and understanding. All of JMI's work with young audiences is based on the underlying principal that all children and youth should receive access to music/culture as a fundamental human right. Thus, although in many nations we now celebrate an improvement in the music programs of education institutions, the YAMA serves as a beacon of hope to those still facing less than desirable circumstances, to continue the fight for this crucial sector of human development.

YAMA is a JMI Young Audiences Working Group Initiative

More info:

Matt Clark
Communications Officer
Jeunesses Musicales International
matt@jmi.net

T. +32 2 513 97 74

Jeunesses Musicales International (JMI) is the world's largest youth-music NGO. With a mission "to enable young people to develop through music across all boundaries," JMI reaches over 5 million young people aged 13-30 annually through 36,000 activities and is the leading organization in the field of young audiences.


Thursday, February 4, 2010

Mara nyingine mtu unaweza kuanza kupata picha kama vile wanamuziki wako Dar es Salaam tu, jambo ambalo si kweli. Japo ukweli ni kuwa zamani kulikuweko na Bendi karibu kila wilaya nchini. Hapa ni bendi 2 kutoka Dodoma. Super Melody na Saki Stars.
Mwenye gitaa na jaketi la rangi mbili ni Mzee Ikunji, huyu pamoja na kupigia bendi kama Tabora Jazz pia alikuweko Tancut Almasi Orchestra na ndie aliyepiga second solo kwenye nyimbo kama Masafa Marefu, Nimemkaribisha nyoka, na Kashasha

Hii ni Bendi inayoitwa Karafuu Band,moja ya bendi kadha wa kadha zilizo na masikani Zanzibar. Mwenye miwani ya jua ndio kiongozi wa bendi anaitwa Anania Ngoliga, ni mwanamuziki mwenye ulemavu wa macho lakini kati ya wanamuziki mahiri Tanzania. Anania ambaye kwa wakati huu yuko Marekani katika tour ambayo anasindikizana na mwanamuziki Bela Fleck. Fleck amepata grammy awards 3 mwaka huu. Na katika album iliyopata awards kuna nyimbo 2 ambazo zimetungwa na Anania. Anania kisha kuwa mwanamuziki katika bendi ya Legho Stars, Afrisongoma, Tango Stars, Tacosode Band. Amesharekodi na wanamuziki wengi mahiri wakimataifa akiwemo Kriss Kristoffeson, na Zapmama


Hapa kuna wakubwa wawili katika ulimwengu wa soka, Sylersaid Mziray, kocha anaeheshimika sana, na Mzee Hassan Dalali mwenyekiti wa Simba Sports Club enzi hizo akiwa Kiongozi na mpigaji solo wa bendi ya Vijana Jazz.Mziray alikuwa katembelea Kilimanjaro Band wananjenje.

Kati ya mwanamuziki Mtanzania ambae historia hajamtendewa haki kutokana na kutothaminiwa kwa kazi zake ni marehemu Mzee Frank Humprik. Mzee Humprik anaeonekana hapa katika picha ya rangi ameishi kwa miaka mingi ya mwisho wa maisha yake Lushoto. Mzee huyu akiwa na dada zake wawili walitikisa anga za muziki wa Afrika ya Mashariki, na bado wanaendelea kufanya hivyo japo hawatambuliwi kabisa. Kundi lao lililoitwa Frank na dada zake waliuletea ulimwengu nyimbo kama Embe dodo imelala mchangani, Kolokolola, Chaupele Mpenzi na nyingine nyingi ambazo bendi bado zinapiga nyimbo hizo mpaka leo na baadhi ya wanamuziki wamekuwa wanazirekodi bila hata kutaja mtunzi wa nyimbo hizo. Mbaya zaidi mara nyingi nyimbo hizo zimekuwa zikitambulishwa kama nyimbo za mwanamuziki mwingine kutoka Kenya marehemu Fundi Konde.
Mzee Fundi Konde ambae hapa chini yuko na mwanamuziki mwingine maarufu wa Kenya Fadhili William aliyeimba Malaika, ndiye aliyetuachia nyimbo kama Ajali haikingi, Mama Leli, Wekundu si hoja, Mombasa siendi tena na kadhalika

Mzee Frank Humprick


Kati ya mwanamuziki ambae hajatendewa haki kutokana na kutothaminiwa kwa kazi zake ni marehemu Mzee Frank Humprick. Mzee huyu akiwa na dada zake walitunga nyimbo nyingi sana ambazo mpaka leo zinapigwa majukwaani na karibu kila bendi Afrika mashariki. Bendi nyingine zimediriki kurekodi upya nyimbo hizo tena bila hata kumtaarifu Mzee huyu au nduguze. Baya zaidi ni nyimbo zake nyingi kutambulishwa kuwa ni za Fundi Konde. Nyimbo zake kama Embe dodo imelala mchangani, Chaupele mpenzi,I am a democrat(uliopigwa marufuku wakati wa mkoloni),Kolokolola na nyingine nyingi. Mzee huyu Mtanzania aliyekuwa akiishi Lushoto mpaka kifo chake anastahili kuenziwa na wapenzi wote wa muziki Tanzania.

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...