YOUTUBE PLAYLIST

Thursday, February 4, 2010

Hii ni Bendi inayoitwa Karafuu Band,moja ya bendi kadha wa kadha zilizo na masikani Zanzibar. Mwenye miwani ya jua ndio kiongozi wa bendi anaitwa Anania Ngoliga, ni mwanamuziki mwenye ulemavu wa macho lakini kati ya wanamuziki mahiri Tanzania. Anania ambaye kwa wakati huu yuko Marekani katika tour ambayo anasindikizana na mwanamuziki Bela Fleck. Fleck amepata grammy awards 3 mwaka huu. Na katika album iliyopata awards kuna nyimbo 2 ambazo zimetungwa na Anania. Anania kisha kuwa mwanamuziki katika bendi ya Legho Stars, Afrisongoma, Tango Stars, Tacosode Band. Amesharekodi na wanamuziki wengi mahiri wakimataifa akiwemo Kriss Kristoffeson, na Zapmama

No comments:

Post a Comment

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...