YOUTUBE PLAYLIST

Monday, July 5, 2010

Orchestra Mambo Bado





Orchestra Mambo Bado ilikuwa bendi ambayo haikukaa kwa muda mrefu katika anga za muziki. Bendi hii ilianza mwaka 1981, ikiwa chini ya 'Mtoto Mzuri' Tchimanga Assossa ikajulikana sana kwa ajili na mtindo wake ulioitwa Bomoa Tutajenga kesho. Pichani Sadi Mnala Drums (yuko Msondo), William Maselenge rythm guitar(marehemu), Andre Milongo(?), Bass na Second Solo, Kazembe wa Kazembe(marehemu) Solo guitar. Pamoja nao walikuweko John Kitime(Njenje), Jenipher Ndesile (?), George Mzee(Marehemu), Likisi Matola(Moonlight Band),Lucas Faustin(Police Brass Band) na Huluka Uvuruge(Msondo), baadae Athumani Cholilo(Marehemu) na Banza Tax(Marehemu), Selemani Nyanga(Uholanzi), Nana Njige(Marehemu). Wimbo wao Bomoa Tutajenga Kesho ulipigwa marufuku.

Saturday, July 3, 2010

The Djs

Hii picha ni kumbukumbu kubwa katika ulimwengu wa Disco Tanzania. Pichani ni kati ya the most bfamous Djs Tanzania wakati huo. Najua wadau mtawataja wote hapa, Meb, Masoud Masoud, John Peter, .................

Wednesday, June 30, 2010

Stage Shows

Taratibu za akina mama kucheza show zilikuwa zikienda sambamba na shughuli nyingine za muziki kwa miaka mingi sana. Nimebahatika kukutana na akina mama wawili ambao walikuwa katika ngazi za juu za uchezaji miaka hiyo. Chini kushoto ni Maida Lwambo, yeye alianza shughuli za sanaa 1973, katika kikundi cha sanaa cha Magereza akishiriki , sarakasi na maigizo, mwaka 1977 akahamia kikundi cha sanaa cha Urafiki akiwa kama muimbaji katika kwaya, na mwaka 1979 hadi 1981 alikuwa akicheza show Orchestra Maquis Original, akahamia kwa miezi michache kwa Doctor Remmy,kisha kati ya 1985 mpaka 1988 alikuwa Orchestra Safari Sound(Dukuduku), na hatimae akarudi Maquis mpaka alipostaafu kucheza show. Kulia ni Anna Mganga, alieanza sanaa katika kikundi cha Tanzania Breweries mwaka 1974,akajiunga na kundi la sanaa la Bora Shoes, na hatimae mwaka 1981 akajiunga na Maquis, kwa muda mfupi mwaka 1983 alihamia OSS, lakini alirudi tena Maquis mbapo alikaa mpaka 1993, alipoacha kucheza show. Hawa wadada walikuwa ndio wanatikisa jiji katika fani yao miaka hiyo.

Tuesday, June 22, 2010

Saba saba..............

KWA KWELI KILA TUKIMALIZA MAZOEZI NATOKA NIMEFARIJIKA KUWA TANZANIA TUNA WANAMUZIKI WA KIWANGO CHA JUU ILA TARATIBU ZETU NDIO MBAYA. KWA WALE WATAKAOHUDHURIA ONYESHO LA HAWA WANAMUZIKI WAKONGWE WATAONA NINI MAANA YA NINACHOSEMA. NA LA KUSIKITISHA NI AINA YA MUZIKI UNAOPIGWA HAPA NAONA NDIO UKO UKINGONI KUONDOKA NA WAZEE HAWA

Sabasaba........

Mazoezi yanaendelea kwa nguvu .





Masoud Masoud alipita kujionea

King Kiki na Bi Shakila....what a combination!!!!!!!


King Kiki, Shakila, Bitchuka

Sunday, June 20, 2010

Disco

Haya djs walikuwa, na bado ni watu muhimu katika shughuli za muziki Tanzania, labda nikupe maelezo mafupi. Baada ya Biribi kupumzika, akazuka kijana huyu, kwanza kwenye parties maeneo ya Upanga, na baadae kuwa dj maarufu aliyejulikana kama Dj Emperor, akiburudisha sana pale Agip Motel na kisha kuhamia ghorofa ya saba New Africa Hotel, alifanya mambo makubwa Arusha pia wapenzi wa disco mnamkumbuka? na disko lake liliitwaje?




Friday, June 18, 2010

Tancut almasi Orchestra enzi hizo

Tancut Almasi katika onyesho mojawapo. Hawa dada wawili, ni Nana Njige(marehemu), na Nuru Mhina ambaye baadae aliolewa na Kabeya Badu ambaye ni muimbaji katika bendi ya Wazee Sugu. Trumpet Ray Mlangwa magitaa John Kitime na Kawelee Mutimwana,

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...