YOUTUBE PLAYLIST
Friday, July 29, 2022
TWANGA PEPETA KISIMA CHA BURUDANI KILA IJUMAA MAWASILIANO PARK
Vokali kali toka kwa Charles Baba Kingunge, akiwa na wakali wenzake wa Twanga Pepeta Sugu Kisima cha Burudani, kila Ijumaa huwa zinasikika Mawasiliano Park Ubungo jirani kabisa na jengo yalipo Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania yaani TCRA kuanzia saa mbili kamili usiku. Unakosaje?
Thursday, July 28, 2022
Wednesday, July 27, 2022
RATIBA YA BONGO BEATS BAND
ALHAMISI --- KIBOZONE MARAMBA MAWILI MBEZI
IJUMAA--- KALAMBEZI BAR UBUNGO TANESCO
JUMAMOSI --- MAGIC LOUNGE KWA LIPELANYA MBEZI MSAKUZI
JUMAPILI ---DAGAA DAGAA UBUNGO KIBO
KARIBUNI WAPENZI WETU,
BABA AMEONDOKA MTOTO AMEBAKI, KAMA ZAMANI.
Tuesday, July 26, 2022
DEKULA BAND YASHIRIKI FEST AFRIKA FESTIVAL YA FINLAND
Dekula Kahanga Vumbi na Menard Mponda mara baada ya onyesho la nguvu la Dekula Band |
Bendi kongwe yenye maskani yake katika jiji la Stockholm kule Sweden, siku ya tarehe 18 Juni 2022 ilitumbuiza katika tamasha la Kimataifa la Fest Afrika Festival, lililofanyika Tampere Finland.
Tamasha hili linalo endeshwa na Mtanzania anaeishi Finland, Bwana Menard Mponda, ni tamasha la miaka mingi, ambalo limewahi kualika hata bendi kadhaa kutoka Tanzania zikiwemo Yamoto Band na Extra Bongo Band.
Dekula Band jukwaani.
Kwa habari zaidi za tamasha la Fest Afrika Festival ingia
FESTAFRIKA
SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...
-
Mara baada ya kutoa ule wimbo maarufu wa Kisambaa Shakaza, Eddy Sheggy mwenyewe na Wasambaa wengine wakaanza kuitwa Shakaza. Eddy Sheggy ali...
-
Suleiman Mbwembwe, aliyekuwa anajulikana pia kwa jina la Electronic Voice, alikuwa mwimbaji na mtunzi aliyeng'ara katika enzi zake. Aki...
-
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...