YOUTUBE PLAYLIST

Sunday, July 11, 2010

SITI BINTI SAAD


Kwa kila hali Siti Binti Sadi anastahili kuenziwa. Kwa akina mama, mwanamke huyu shujaa aliyetoka katika familia maskini ya kijijini, ataenziwa kwa kuwa aliweza kushinda mfumo uliokuwa ukizuia wanawake kujichagulia mfumo wa maisha yao, na kuweza kujitokeza kufanya yale ambayo hayakuwezekana kwa mwanamke wa aina yake kabla. Alijitokeza na kuwa mwanamke mwimbaji mwenye nguvu za kuendesha shughuli za muziki katika mfumo uliotawaliwa na wanaume.

Kwa akina mama wanamuziki katika Taarabu, alikuwa ndio ufunguo ya mfumo uliopo ambao taarab inaongozwa na waimbaji wa kike.

Alikuwa ndie mwasisi wa kuimba taarab kwa Kiswahili.

Kwa wanamuziki wote kwa ujumla Siti Binti Sadi ni super star wa kweli.

- Alirekodi santuri zaidi ya 150

- Alikuwa wa kwanza kwenda kurekodi nyimbo zake India May 1928

- Umaarufu wake ulisababisha Columbia Records kujenga studio Zanzibar katika enzi yake ili tu kumrekodi.

Oktoba 1936 aliwahi kufanya onyesho moja huko Pangani na kupata shilingi 1200. Kwa thamani ya pesa wakati ule, mtu aliweza kupanga chumba kwa shilingi 1 kwa mwezi. Na Pangani ilikuwa na wastani wa watu 1500. Si rahisi msanii yoyote wa leo hapa nchini kuweza kufikia Usuper Star huo.

Siti alizaliwa mnamo mwaka 1880 na kufariki 1950.

Wednesday, July 7, 2010

Live photoz Wakongwe concert









We made it pamoja na very strange things happening on the way

Sabasaba........

Hayawi hayawi leo yatakuwa , Wanamuziki na Djs wakongwe leo watakuwepo Karimjee Hall kwa masaa 6 mfululizo,Nimemuona DJ Cedou, DJ John Peter wakiwa na Lps na turntables tayari kuonyesha walichokuwa wakikifanya enzi zao. Maelezo zaidi baadae.

Monday, July 5, 2010

Orchestra Mambo Bado





Orchestra Mambo Bado ilikuwa bendi ambayo haikukaa kwa muda mrefu katika anga za muziki. Bendi hii ilianza mwaka 1981, ikiwa chini ya 'Mtoto Mzuri' Tchimanga Assossa ikajulikana sana kwa ajili na mtindo wake ulioitwa Bomoa Tutajenga kesho. Pichani Sadi Mnala Drums (yuko Msondo), William Maselenge rythm guitar(marehemu), Andre Milongo(?), Bass na Second Solo, Kazembe wa Kazembe(marehemu) Solo guitar. Pamoja nao walikuweko John Kitime(Njenje), Jenipher Ndesile (?), George Mzee(Marehemu), Likisi Matola(Moonlight Band),Lucas Faustin(Police Brass Band) na Huluka Uvuruge(Msondo), baadae Athumani Cholilo(Marehemu) na Banza Tax(Marehemu), Selemani Nyanga(Uholanzi), Nana Njige(Marehemu). Wimbo wao Bomoa Tutajenga Kesho ulipigwa marufuku.

Saturday, July 3, 2010

The Djs

Hii picha ni kumbukumbu kubwa katika ulimwengu wa Disco Tanzania. Pichani ni kati ya the most bfamous Djs Tanzania wakati huo. Najua wadau mtawataja wote hapa, Meb, Masoud Masoud, John Peter, .................

Wednesday, June 30, 2010

Stage Shows

Taratibu za akina mama kucheza show zilikuwa zikienda sambamba na shughuli nyingine za muziki kwa miaka mingi sana. Nimebahatika kukutana na akina mama wawili ambao walikuwa katika ngazi za juu za uchezaji miaka hiyo. Chini kushoto ni Maida Lwambo, yeye alianza shughuli za sanaa 1973, katika kikundi cha sanaa cha Magereza akishiriki , sarakasi na maigizo, mwaka 1977 akahamia kikundi cha sanaa cha Urafiki akiwa kama muimbaji katika kwaya, na mwaka 1979 hadi 1981 alikuwa akicheza show Orchestra Maquis Original, akahamia kwa miezi michache kwa Doctor Remmy,kisha kati ya 1985 mpaka 1988 alikuwa Orchestra Safari Sound(Dukuduku), na hatimae akarudi Maquis mpaka alipostaafu kucheza show. Kulia ni Anna Mganga, alieanza sanaa katika kikundi cha Tanzania Breweries mwaka 1974,akajiunga na kundi la sanaa la Bora Shoes, na hatimae mwaka 1981 akajiunga na Maquis, kwa muda mfupi mwaka 1983 alihamia OSS, lakini alirudi tena Maquis mbapo alikaa mpaka 1993, alipoacha kucheza show. Hawa wadada walikuwa ndio wanatikisa jiji katika fani yao miaka hiyo.

Tuesday, June 22, 2010

Saba saba..............

KWA KWELI KILA TUKIMALIZA MAZOEZI NATOKA NIMEFARIJIKA KUWA TANZANIA TUNA WANAMUZIKI WA KIWANGO CHA JUU ILA TARATIBU ZETU NDIO MBAYA. KWA WALE WATAKAOHUDHURIA ONYESHO LA HAWA WANAMUZIKI WAKONGWE WATAONA NINI MAANA YA NINACHOSEMA. NA LA KUSIKITISHA NI AINA YA MUZIKI UNAOPIGWA HAPA NAONA NDIO UKO UKINGONI KUONDOKA NA WAZEE HAWA

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...