YOUTUBE PLAYLIST
Monday, May 31, 2010
SABA SABA 2
Wanamuziki kadhaa wa zamani walikutana kuongela onyesho la wanamuziki wa zamani litakalofanyika siku ya Sabasaba. Mazoezi yataanza wiki ijayo. Pichani toka juu, Muhidin gurumo, Abdul Salvador, King Kiki na Rehani Bitchuka, Kabeya Badu na Ally Jamwaka, Jeff
Thursday, May 27, 2010
Mayaula Mayoni hatunae tena
Mayaula mayoni si jina geni kwa Watanzania. Pamoja na kuwa mwanamuziki mtunzi katika lile kundi maarufu la TP OK Jazz,chini ya Franco Luambo, Mayaula aliwahi kuwa mchezaji wa Young Africans. Mayaula alikuwa msomi mzuri wa Teknolojia ya Computer. Kwa miaka mingi karibuni alikuwa akaiishi Magomeni Mikumi Dar Es Salaam, huku akifanya kazi Ubalozi wa nchi yake hapa Tanzania.
Mayaula amefariki asubuhi ya tarehe 26 May 2010 huko Brussel Ubelgiji. Alikuwa na miaka 64. Mungu amlaze peponi pema. Sikiliza tungo yake hii akiwa na TP OK Jazz.
Mayaula amefariki asubuhi ya tarehe 26 May 2010 huko Brussel Ubelgiji. Alikuwa na miaka 64. Mungu amlaze peponi pema. Sikiliza tungo yake hii akiwa na TP OK Jazz.
Wednesday, May 26, 2010
Shakaza Eddy Sheggy
Mara baada ya kutoa ule wimbo maarufu wa Kisambaa Shakaza, Eddy Sheggy mwenyewe na Wasambaa wengine wakaanza kuitwa Shakaza. Eddy Sheggy alikuwa mwimbaji mzuri na mtunzi mzuri sana. Kati ya bendi alizopitia ni Super Rainbow, Vijana Jazz, Bantu Group, Washirika Stars. Picha mbili za juu ni Eddy akifanya onyesho na Super Rainbow katika uwanja wa Mnazi Mmoja, chini ni wakati akiwa Vijana Jazz
SABA SABA
Ile siku ya kuvaa slimfit,jackson 5, raizon na muziki ulioendana na kipindi hicho inazidi kukaribia. Vikao vya matayarisho vinaendelea. Wanamuziki ambao watapanda jukwaani siku hiyo ni wale wa enzi zile na kupiga muziki wa enzi zao, tunategemea kusikia wakongwe hao wakiporomosha muziki kutoka sehemu mbalimbali za dunia. Pichani ni washiriki wa kikao kilichoendelea leo 26/5/2010. Waliohudhuria Waziri Ally,Ahmad Dimando, Juma Ubao,Crispin Stephan, Godfrey Mahimbo,Kanku Kelly, Jerry Tom, John Kitime.
Sunday, May 23, 2010
Patrick Pama Balisidya
Mwaka 1996 kwa ufadhili wa Ubalozi wa Netherlands lilifanyika tamasha kubwa la muziki Mnazi Moja, bendi kama Vijana Jazz, Polisi Jazz, Zaita Muzika, Maquis Original, Namtu Group, Shikamoo Jazz, zilishiriki. Hapa Patrick akishirikiana na Vijana Jazz, nyuma yake ni Fred Benjamin mwimbaji wa sauti ya kwanza Vijana Jazz, ambae naye ametangulia mbele ya haki. Siku hii alipiga wimbo wa Ni mashaka na hangaiko akishirikiana na Shikamoo Jazz
Subscribe to:
Posts (Atom)
SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...
-
Mara baada ya kutoa ule wimbo maarufu wa Kisambaa Shakaza, Eddy Sheggy mwenyewe na Wasambaa wengine wakaanza kuitwa Shakaza. Eddy Sheggy ali...
-
Suleiman Mbwembwe, aliyekuwa anajulikana pia kwa jina la Electronic Voice, alikuwa mwimbaji na mtunzi aliyeng'ara katika enzi zake. Aki...
-
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...