
Kwa wapenzi wa Fauvette na baadae Kasheba Group na Zaita Muzika, sauti ya Baziano si rahisi kusahaulika. Lakini kwa mapenzi yake Mungu, Baziano(wa kwanza kushoto) na mpiga gitaa wake Ndala Kasheba (wa pili kutoka kulia) hatunao tena duniani Mungu awalaze pema peponi. Pichani pia yupo Kasongo Mpinda (mwimbaji) wa pili kushoto, na Matei Joseph (mpiga drums).
Namkumbuka Kasongo Mpinda ''Clayton.'' Miaka ya mwisho kabla utandawazi alikuwa Mk Group, Ngoma za maghorofani, akitamba na wimbo wake Kibera. . . Kibera acha chuki, chuki yavunja unyumba eeh...ooh kibera eeh, kibera eeh mama kibera.. Those old good days, bwana!
ReplyDelete