YOUTUBE PLAYLIST
Wednesday, July 7, 2010
Sabasaba........
Hayawi hayawi leo yatakuwa , Wanamuziki na Djs wakongwe leo watakuwepo Karimjee Hall kwa masaa 6 mfululizo,Nimemuona DJ Cedou, DJ John Peter wakiwa na Lps na turntables tayari kuonyesha walichokuwa wakikifanya enzi zao. Maelezo zaidi baadae.
Monday, July 5, 2010
Orchestra Mambo Bado
Orchestra Mambo Bado ilikuwa bendi ambayo haikukaa kwa muda mrefu katika anga za muziki. Bendi hii ilianza mwaka 1981, ikiwa chini ya 'Mtoto Mzuri' Tchimanga Assossa ikajulikana sana kwa ajili na mtindo wake ulioitwa Bomoa Tutajenga kesho. Pichani Sadi Mnala Drums (yuko Msondo), William Maselenge rythm guitar(marehemu), Andre Milongo(?), Bass na Second Solo, Kazembe wa Kazembe(marehemu) Solo guitar. Pamoja nao walikuweko John Kitime(Njenje), Jenipher Ndesile (?), George Mzee(Marehemu), Likisi Matola(Moonlight Band),Lucas Faustin(Police Brass Band) na Huluka Uvuruge(Msondo), baadae Athumani Cholilo(Marehemu) na Banza Tax(Marehemu), Selemani Nyanga(Uholanzi), Nana Njige(Marehemu). Wimbo wao Bomoa Tutajenga Kesho ulipigwa marufuku.
Saturday, July 3, 2010
The Djs
Wednesday, June 30, 2010
Stage Shows
Taratibu za akina mama kucheza show zilikuwa zikienda sambamba na shughuli nyingine za muziki kwa miaka mingi sana. Nimebahatika kukutana na akina mama wawili ambao walikuwa katika ngazi za juu za uchezaji miaka hiyo. Chini kushoto ni Maida Lwambo, yeye alianza shughuli za sanaa 1973, katika kikundi cha sanaa cha Magereza akishiriki , sarakasi na maigizo, mwaka 1977 akahamia kikundi cha sanaa cha Urafiki akiwa kama muimbaji katika kwaya, na mwaka 1979 hadi 1981 alikuwa akicheza show Orchestra Maquis Original, akahamia kwa miezi michache kwa Doctor Remmy,kisha kati ya 1985 mpaka 1988 alikuwa Orchestra Safari Sound(Dukuduku), na hatimae akarudi Maquis mpaka alipostaafu kucheza show. Kulia ni Anna Mganga, alieanza sanaa katika kikundi cha Tanzania Breweries mwaka 1974,akajiunga na kundi la sanaa la Bora Shoes, na hatimae mwaka 1981 akajiunga na Maquis, kwa muda mfupi mwaka 1983 alihamia OSS, lakini alirudi tena Maquis mbapo alikaa mpaka 1993, alipoacha kucheza show. Hawa wadada walikuwa ndio wanatikisa jiji katika fani yao miaka hiyo.
Tuesday, June 22, 2010
Saba saba..............
KWA KWELI KILA TUKIMALIZA MAZOEZI NATOKA NIMEFARIJIKA KUWA TANZANIA TUNA WANAMUZIKI WA KIWANGO CHA JUU ILA TARATIBU ZETU NDIO MBAYA. KWA WALE WATAKAOHUDHURIA ONYESHO LA HAWA WANAMUZIKI WAKONGWE WATAONA NINI MAANA YA NINACHOSEMA. NA LA KUSIKITISHA NI AINA YA MUZIKI UNAOPIGWA HAPA NAONA NDIO UKO UKINGONI KUONDOKA NA WAZEE HAWA
Sabasaba........
Subscribe to:
Posts (Atom)
SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...
-
Hawa ndio The Jets (1972), ambao baadae walikuja kuwa STC Jazz, ambayo ndio chanzo cha Biashara Jazz. Waliopo hapa wa kwanza Belino, Raphael...
-
Mara baada ya kutoa ule wimbo maarufu wa Kisambaa Shakaza, Eddy Sheggy mwenyewe na Wasambaa wengine wakaanza kuitwa Shakaza. Eddy Sheggy ali...
-
Suleiman Mbwembwe, aliyekuwa anajulikana pia kwa jina la Electronic Voice, alikuwa mwimbaji na mtunzi aliyeng'ara katika enzi zake. Aki...