YOUTUBE PLAYLIST

Thursday, February 4, 2010


John Mwenda Bosco,ni kati ya wanamuziki ambao w alileta mabadiliko mengi katika muziki wa Afrika ya Mashariki. Muziki wake unapendwa sana mpaka leo. Je unajua alikuwa nani?

Peter Colmore ambaye alifanya kazi kwa karibu sana na Mzee Ally Sykes ambaye kwa bahati mbaya hajatunukiwa nafasi anayostahili katika historia ya muziki wa Tanzania ndie aliye mleta John Mwenda Bosco Afrika ya Mashariki. Bosco alitambulishwa kwa Colmore kupitia Edward Masengo,mwanamuziki mwingine toka Kongo ambae alikuwa maarufu sana na hasa kutokana na matangazo ya biashara yaliyokuwa yanafanywa na kampuni ya Colmore na Mzee Sykes, Colmore akalazimika kumfuata Bosco hadi Congo ambapo serikali ya Kibergiji wakati huo ilimlazimisha alipe Faranga 30,000 kama pesa ya kuhakikisha atamrudisha Bosco kwao. Bosco alikuwa tayari anajulikana sana Afrika ya Mashariki kupitia santuri zake. Kati ya nyimbo maarufu za Bosco ni ule wimbo wa ala tupu ambao hutumika na Radio Tanzania kuashiria kuanza kwa kipindi cha zilipendwa.

Taarab
Muziki wa Taarab unautata wa vyanzo viwili. Kuna wanaosema taarab iliingia nchini mwetu kupitia ikitokea Mombasa. Kuna tafiti nyingine ambazo zinaonyesha Sultan Barghash wa Zanzibar aliwapeleka wanamuzikiwawili Misri kujifunza upigaji wa Taarab,na hao waliporudi ndo walipanda mbegu ya Taarab nchini mwetu. Taarab imekuwa nahistoria ambayo ya kuwa na aina nyingi za taarab, na mpaka leo mabadiliko ya taarab yanaendelea. Imefikia sasa kuna hata vikundi vya taarab vina wacheza show. Taarab imekuwa pia ni ya kucheza na si kusikiliza ujumbe tu kama ilivyokuwa zamani

Wednesday, February 3, 2010

Extra Bongo ya Ally Choky kazini







Vijana Jazz Band wakisubiri kupiga muziki katika siku ya kumpokea Mzee Nelson Mandela mara baada ya kuachiwa kifungoni, hapa wakiwa stadium Morogoro. Toka kushoto waliosimama John Kitime kwa sasa yupo Kilimanjaro Band, Marehemu Agrey Ndumbalo, Mhasibu wa Bendi, Abou Semhando yupo African Stars (Twanga Pepeta),Marehemu Fred Benjamin, Said Mnyupe yuko Msondo,Said Mohamed Ndula, Rashid Pembe anendelea na muziki Mak Band, Hassan Show yupo Malasyia na Kinguti System wakipiga muziki huko. Waliokaa mpenzi wa bendi, marehemu Bakari Semhando, Juma Choka yupo sikinde.

Picha ya chini, Mohammed Gotagota, Freddy Benjamin,Mhando,Said Mohamed 'Ndula',Rashid Pembe,Aggrey Ndumbalo, hiyo ndo Vijana Jazz Saga Rhumba


Tancut Almasi Orchestra, bendi iliyokuwa namakazi yake Iringa kuanzia 1987, ilikuwa chini ya Kiwanda cha kuchonga almasi cha hapo Iringa, Diamond Cutting Company. Bahati mbaya wengi ni marehemu. Kutoka kushoto Buhero Bakari inasemekana ni mganga wa dawa za asili kwa sasa,marehemu Kyanga Songa, Kasaloo Kyanga yupo Dar anaendelea na muziki,Kabeya Badu, yuko na King Kiki na wazee sugu, Marehemu Kalala Mbwebwe, Abdul Mngatwa, yuko Iringa ameacha muziki, Akuliake Salehe aka King Maluu yupo Dar anaendelea na muziki

Tuesday, February 2, 2010

Hao si wengine bali ni wanamuziki wa The Revolutions, ambayo sasa inajulikana kama The Kilimanjaro Band aka Wananjenje. Pichani kutoka kushoto, Juma Omary(Drums/uimbaji),Mohammed Mrisho (Gitaa/uimbaji), Mabrouk Omary( Mwimbaji), Waziri Ally (Keyboards/ uimbaji), Marehemu Chuky,Keppy Kiombile(Bass /Uimbaji).Tangazo mojawapo la Kilimanjaro Band katika moja ya safari za Oman

UMUHIMU WA KULIPIA MATUMIZI YA MUZIKI

Ukitunga wimbo na ukiiweka katika hali ya kushikika mara hiyo unaanza kupata haki zote za wimbo hiyo. Wimbo ni mali itokananyo na ubunifu hivyo moja kwa moja unapata haki zinazostahili kutokana na mali hiyo na ni mali yako kama vile mali nyingine. Mara wimbo utakapokuwa tayari kutumika ni muhimu kusajili katika sehemu husika ili uweze kupata ulinzi na stahili zitakazopatikana kutokana na mali hiyo. Kuna haki za aina mbili, Performance Rights na Mechanical Rights.

Performance Rights ni zile haki zitokanazo na tungo ya muziki kutumika hadharani au kurushwa hewani. Hii inajumlisha pamoja na muziki kupigwa na Live Band na, au hata muziki uliokwisha rekodiwa kupigwa hadharani katika sehemu za hadhara kama restaurants, bar, klabu za usiku, kwenye maharusi, na kadhalika. Performance rights pia ni haki zinazoambatisha muziki kurushwa hewani kupitia radio na televisheni. Kutokana na kuweko kwa haki hizi, watu binafsi na makampuni ambayo yangependa kutumia kazi hizo ni lazima wapate ruksa kwa mwenye mali na hivyo mwenye wimbo kupata royalties kila wimbo wake unaporushwa hewani au kutumika hadharani.

Mechanical Rights ni zile haki zinazohusiana na kuweka tungo katika vinasa sauti kama vile kanda CD na DVD. Hivyo mtu au kampuni inapotaka kuweka kazi ya mtu katika kinasa sauti cha aina yoyote kutalazimika kuwepo na ruksa kutoka kwa mwenye mali au taasisi ambayo ina mamalaka ya Mechanical Rights za kazi hiyo. Watunzi hupata Mechanical Rights kwa nyimbo zinaposambazwa na wauzaji.

Ili kurahisisha ufuatiliaji na uratibu wa haki zilizotajwa hapo juu copyright collecting agency au copyright collecting society hutengenezwa ambapo aidha huwa ni chombo kilichobuniwa na watunzi au chombo kilichowekwa kisheria. Chombo hiki hupewa mamlaka na wanachama pia kutoa na kusimamia leseni mbalimbali kwa kazi walizozisajiri

Kwa hapa Tanzania Bara chombo ni COSOTA na Zanzibar COSOZA. Hivi ni vyombo vilichopewa mamlaka kisheria kushughulika kwa niaba ya watunzi kufuatilia haki zao, na kukusanya mafao yatokanayo na kazi hizo.

Ujio wa vinasa sauti bora na mtandao wa intanet unawezesha mamilioni ya watu kuweza kusikiliza wimbo kwa wakati mmoja katika maeneno mbalimbali ulimwenguni. Siyo siri kuwa matumizi kama ringtones ni biashara kubwa sana ambayo wasanii hawajapata manufaa stahili kutokana na mapato ya kazi zao.

Kuweko kwa taratibu za kukusanya mirabaha kuna wapatia fulsa wanamuziki wakongwe kuendelea kupata chochote na hata kutajirika japo nyimbo zao ni za zamani, napengine haziuziki tena. Mtunzi wa wimbo wa Red red wine alikwisha kata tama kimaisha uliporekodiwa upya wimbo huo ametajirika kutokana na wimbo huo.

Kuweko kwa vinasa sauti kumepunguza umuhimu wa kuweko kwa live music, hivyo malipo ya mirabaha inawezesha wanamuziki kupata mafao yao kwa kazi zao zilizotumika badala ya wao. Ni ukweli usiopingika kuwa kuna baadhi ya shughuli haziwezi kukamilika bila ya matumizi ya muziki. Kwa mfano biashara nyingi huongezea motisha kwa kupiga muziki. Mabaa, restaurant, magari ya kusafirisha abairia, na kadhalika. Haya ni matumizi makubwa tu ya muziki.

Shughuli mbali mbali za sherehe kama vile mikutano ya kisiasa, harusi birthday party hutawaliwa na muziki ambao matumizi yake huwa hayalipiwi kinyume kabisa cha haki za kimsingi za binadamu waliotunga nyimbo zinazotumika

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...