YOUTUBE PLAYLIST

Friday, April 23, 2010

Bendi za Mkoa wa Morogoro

Kati ya mikoa iliyokuwa na Bendi nyingi, sijui kama ulikuweko ulioushinda mkoa wa Morogoro. Ilikuwa kila wilaya ina bendi. Baadhi ya bendi ninazozikumbuka ni Morogoro Jazz, Super Volcano, Cuban Marimba Band, Les Cuban, TK Limpopo, Kilosa Jazz (alikotokea Abel Balthazar), Ifakara Jazz, Sukari Jazz, Imalinyi Jazz, Mahenge Jazz, Kwiro Jazz., Mzinga Troupe. Na hata wale wakali wa wakati huo na ule wimbo wao enye maneno,

Waache waseme watachoka wao,

Mzee Makelo endeleza libeneke,

Waache waseme watachoka wao,

mtindo libeneke unatia fora

Hapa naongelea Butiama Jazz Band, iliyokuwa inapiga muziki kwa mtindo wao uliotokana na ngoma ya kwao Libeneke,wao ni wa Ifakara hivyo nao ni bendi ya mkoa wa Morogoro japo jina lilitokana na mahala alipozaliwa Baba wa Taifa.(Mzee Mkwega aliyekuwa mwenye bendi alikuwa kada mzuri sana wa CCM, hata kifo chake kilimkuta akiwa mtumishi wa CCM ofisi ndogo Dar es Salaam).

Mpaka leo ukienda Ifakara wakati wa msimu wa mavuno ikiwa kuna sherehe za jumla kama vile kipaimara, ndo utajua wanavyopenda ngoma. Kuna vikundi vingi vya ngoma ya Sangula na kila kikundi kimejipa jina la Bendi, hivyo utakuta mabango yakitangaza Tancut Almasi, Msondo, Super Volcano, na kila nyumba yenye sherehe huandaa kundi lake ni raha tupu hapo

Tuesday, April 20, 2010

Those were the days


Those were the days my friend,
We thought they would never end,
We would sing and dance for ever and a day.
We'd live the life we chose,
We'd fight and never loose ,
Cause we were young O yes we were young. Katika picha.. Patrick Balisidya na Salim Willis enzi za Afro 70

The Rifters 2


Kuna mara nyingine nakosa la kusema nikifikiria hali iliyopo katika ulimwengu wa muziki leo hapa Tanzania. Akina Raphael walikuwa wanawaza nini wakati wanapiga hapa? na ilikuwa nyimbo gani? wanaonekana wana mawazo hawa ni The Rifters

Shaaban Yohana Wanted


Nilikutana na Shaaban Yohana kwa mara ya kwanza katika bendi ya Tancut, ambapo gitaa lake la solo husikika katika nyimbo zote zilizokuwemo katika album za kwanza za bendi ile. Alipiga gitaa katika nyimbo zifuatazo:-
Nimemkaribisha nyoka
Kashasha
Tutasele
Mtaulage
Masafa Marefu
Butinini. Lakini aliniacha Tancut na kwenda Vijana Jazz huko tukakutana tena ambako solo lake linakumbukwa katika nyimbo nyingi kama vile Aza, Ogopa Tapeli,Thereza, Shoga, Malaine nk. Aliacha bendi ya Vijana na kujiunga na Ngorongoro Heroes akatesa sana huko, kisha akatimkia Botswana ambako yuko mpaka leo, muda mwingi akiutumia kama mwanamuziki wa studio.

The Jets


Hawa ndio The Jets (1972), ambao baadae walikuja kuwa STC Jazz, ambayo ndio chanzo cha Biashara Jazz. Waliopo hapa wa kwanza Belino, Raphael Sabuni, Mgoro katika moja ya maonyesho yao. Marijanio Rajab alijiunga na kundi hili, na kuimba wimbo kama.... Ilikuwa usiku wa manane.

Monday, April 19, 2010

Flaming Stars


Familia ya akina Sabuni ilikuwa maarufu sana katika makundi ya vijana wapenzi wa muziki wa Buggy , John , Cuthbert, Raphael wote walikuwa wanamuziki, na kundi la Flaming Stars lilikuwa ni la akina Sabuni. Katika picha hii ya Flaming Stars unawatambua wangapi.?

Afro70 1974

Afro 70 wakiwa Namanga baada ya kutoka Nairobi kupata vyombo vipya. Walilazimika kupiga Namanga ili wapite na vyombo bila bughudha. Unawakumbuka majina?

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...