
Leo ni Jumapili ngoja nilete picha ambayo kwa vyovyote ilipigwa Jumapili , maana ndio ilikuwa siku ya Buggy, lile dansi la mchana lililokuwa linaanza saa 7 au nane na kuisha saa kumi na mbili jioni. Unaona mavazi ya siku hizo?, si muda mrefu baada yalipigwa marufuku , na kukaweko na posters kila mahala zikionyesha nguo gani za kuvaa. Vijana wa TANU Youth League walikuwa wakitembea na mikasi na kuchana nguo zilizoonekana hazifai. Loh, Hawa Rifters walikuwa kati ya makundi mengi ya wanamuziki vijana waliokuwa wakipiga muziki wa soul, hapa bwana nyimbo za Otis Redding, Kipofu Clarence Carter, Wilson Pickett , James Brown,Sam and Dave, Isaac Hayes ilikuwa mwendo mdundo
clarence carter dont you know this is another man's wife? Patches! hayo ndiyo yalikuwa mambo
ReplyDeleteClarence Carter.. Too weak to fight,Getting the bills
ReplyDeleteJohn na Percy Sledge je? 'When a man loves a woman'na 'Give me Your warm and tender love'. Wow wow maan. That was great brother!!Cause you get that soul feelin' maan. Hahaha
ReplyDeleteTake time to know her, Ave Maria, On the dark end of the street
ReplyDelete