YOUTUBE PLAYLIST

Wednesday, July 7, 2010

Live photoz Wakongwe concert









We made it pamoja na very strange things happening on the way

12 comments:

  1. Anonymous12:01

    SERIKALI HAINABUDI KWAANGALIA SWALA HILI,TUMEONA WANAMUZIKI WA INCHI ZOTE WANAPO UNGANA KUSAIDIA JAMII,SERIKALI LAZMA IWASAIDIE.
    OLD SCHOOL TANZANIA WANA JARIBU KWAAMBIA SERIKALI KIVITENDO KWAMBA,MUZIKI WA DANSI UKO NJIANI KUTOWEKA...NAKUOMBENI OLD SCHOOL MSICHOKE KILA MWAKA FANYENI TAMASHA KAMA HILI

    ReplyDelete
  2. Anonymous21:09

    Mkuu,

    Hongereni sana kwa mafanikio.

    Nina hakika mmejifunza mengi ya furaha na huzuni.

    Athari za kutokuwepo sheria/taratibu madhubuti, wataalamu wa itikadi, na mamlaka makini za udhibiti (Strict Regulatory Authorities)chini ya Wizara ya Elimu na Utamaduni zinaanza kuonekana dhahiri. Wengi wa waliopo hawajali wala hawajui.

    Nikiziangalia hizo picha nawasawiri nyie na kina Paul McCatney, Ringo Starr, Mick Jagger, Charlie Watts, Ronnie Wood, Keith Richards, Bob Geldof, David Bowie, na wengine ambao leo ni icon symbols za muziki wa Uingereza. Nawasawiri na kina Joe Cooker, Stevie Wonder, Paul Simon, Quincy Jones, Aretha Franklyn, Kenny Rogers na wanamuziki wengine ambao ndiyo icon symbols za muziki wa Marekani.

    Hata Afrika ya Kusini kina Hugh Masekela, Abdulla Ibrahim, Dorothy Masuka (japokuwa Mzimbabwe), na wengineo wanabebwa kama icon symbols siyo tu za muziki wa Afrika ya Kusini bali mashujaa wa ukombozi dhidi ya utawala wa kibaguzi wa Makaburu.

    Hawa niliowataja na ambao sijawataja ambao wamo katika nasaba moja nao wanathaminiwa sana huko makwao.

    Kwetu soko huria limekuwa huru mno. Hakuna aliyewahi kukaa na kutafakari athari za soko huria kwenye sekta ya muziki. Muziki umeachiwa holela. Kila mwenye vijisenti aidha anakuwa producer, promoter, manager, mmiliki au muhodhi wa wanamuziki au vyombo vya muziki (owners of media outlets). Samahani kwa lugha nitakayoitumia: maamuma wasiojua mbele wala nyuma wameruhusiwa kuwa wasemaji na wahodhi wa muziki na wanamuziki. N

    Tanzania ya leo anakuja mwanamuziki kama Youssous N'dour tunashindwa kuwakusanya wanamuziki ambao wangeweza kumranda kimuziki na hata kisanaa. Hatuna tena wawakilishi ambao wataweza kutuwakilisha kama tulivyowakilishwa Tokyo, Japan mwaka 1974 au Lagos, Nigeria mwaka 1977.

    Si hivyo tu hatuna hata haya wala aibu kupeleka washindani kwenye Kora Award bila kuangalia wale wanaoshiriki kwenye Kora Award ni wanamuziki wa nasaba gani.

    Anyway, kusema sana kunaweza kupotosha maana. Lakini cha msingi ni kwamba tunabomoa ukuta imara na kujenga maboma ya mijiti. Lazima watokee tena kina Chediel Mgonja, Major General Mirisho Sarakikya, Marehemu Godwin Kaduma, Mwalimu Gasper Materu, Marehemu Moses Nnauye, Marehemu Mzee Mayagilo etc etc hapo ndipo tutakasimamia tena national identity.

    Mungu Ibariki Tanzania. Waamshe na watu wake uwape hekima na busara. Amen.

    ReplyDelete
  3. Anonymous21:12

    Mkuu,

    Hongereni sana kwa mafanikio.

    Nina hakika mmejifunza mengi ya furaha na huzuni.

    Athari za kutokuwepo sheria/taratibu madhubuti, wataalamu wa itikadi, na mamlaka makini za udhibiti (Strict Regulatory Authorities)chini ya Wizara ya Elimu na Utamaduni zinaanza kuonekana dhahiri. Wengi wa waliopo hawajali wala hawajui.

    Nikiziangalia hizo picha nawasawiri nyie na kina Paul McCatney, Ringo Starr, Mick Jagger, Charlie Watts, Ronnie Wood, Keith Richards, Bob Geldof, David Bowie, na wengine ambao leo ni icon symbols za muziki wa Uingereza. Nawasawiri na kina Joe Cooker, Stevie Wonder, Paul Simon, Quincy Jones, Aretha Franklyn, Kenny Rogers na wanamuziki wengine ambao ndiyo icon symbols za muziki wa Marekani.

    Hata Afrika ya Kusini kina Hugh Masekela, Abdulla Ibrahim, Dorothy Masuka (japokuwa Mzimbabwe), na wengineo wanabebwa kama icon symbols siyo tu za muziki wa Afrika ya Kusini bali mashujaa wa ukombozi dhidi ya utawala wa kibaguzi wa Makaburu.

    Hawa niliowataja na ambao sijawataja ambao wamo katika nasaba moja nao wanathaminiwa sana huko makwao.

    Kwetu soko huria limekuwa huru mno. Hakuna aliyewahi kukaa na kutafakari athari za soko huria kwenye sekta ya muziki. Muziki umeachiwa holela. Kila mwenye vijisenti aidha anakuwa producer, promoter, manager, mmiliki au muhodhi wa wanamuziki au vyombo vya muziki (owners of media outlets). Samahani kwa lugha nitakayoitumia: maamuma wasiojua mbele wala nyuma wameruhusiwa kuwa wasemaji na wahodhi wa muziki na wanamuziki.

    Tanzania ya leo anakuja mwanamuziki kama Youssous N'dour tunashindwa kuwakusanya wanamuziki ambao wangeweza kumranda kimuziki na hata kisanaa. Hatuna tena wawakilishi ambao wataweza kutuwakilisha kama tulivyowakilishwa Tokyo, Japan mwaka 1974 au Lagos, Nigeria mwaka 1977.

    Si hivyo tu hatuna hata haya wala aibu kupeleka washindani kwenye Kora Award bila kuangalia wale wanaoshiriki kwenye Kora Award ni wanamuziki wa nasaba gani.

    ReplyDelete
  4. Anonymous21:15

    Mkuu,

    Hongereni sana kwa mafanikio.

    Nina hakika mmejifunza mengi ya furaha na huzuni.

    Athari za kutokuwepo sheria/taratibu madhubuti, wataalamu wa itikadi, na mamlaka makini za udhibiti (Strict Regulatory Authorities)chini ya Wizara ya Elimu na Utamaduni zinaanza kuonekana dhahiri. Wengi wa waliopo hawajali wala hawajui.

    Nikiziangalia hizo picha nawasawiri nyie na kina Paul McCatney, Ringo Starr, Mick Jagger, Charlie Watts, Ronnie Wood, Keith Richards, Bob Geldof, David Bowie, na wengine ambao leo ni icon symbols za muziki wa Uingereza. Nawasawiri na kina Joe Cooker, Stevie Wonder, Paul Simon, Quincy Jones, Aretha Franklyn, Kenny Rogers na wanamuziki wengine ambao ndiyo icon symbols za muziki wa Marekani.

    Hata Afrika ya Kusini kina Hugh Masekela, Abdulla Ibrahim, Dorothy Masuka (japokuwa Mzimbabwe), na wengineo wanabebwa kama icon symbols siyo tu za muziki wa Afrika ya Kusini bali mashujaa wa ukombozi dhidi ya utawala wa kibaguzi wa Makaburu.

    Hawa niliowataja na ambao sijawataja ambao wamo katika nasaba moja nao wanathaminiwa sana huko makwao.

    Kwetu soko huria limekuwa huru mno. Hakuna aliyewahi kukaa na kutafakari athari za soko huria kwenye sekta ya muziki. Muziki umeachiwa holela. Kila mwenye vijisenti aidha anakuwa producer, promoter, manager, mmiliki au muhodhi wa wanamuziki au vyombo vya muziki (owners of media outlets). Samahani kwa lugha nitakayoitumia: maamuma wasiojua mbele wala nyuma wameruhusiwa kuwa wasemaji na wahodhi wa muziki na wanamuziki.

    Kusema sana kunaweza kupotosha maana. Nasubiri kusikia yaliyojiri toka kwenu.

    ReplyDelete
  5. Anonymous06:49

    Hapo ilkuwa full vipaji, full legends, full muziki. Bado nasema pamoja na kuwa bado ni kijana, nachagua hii miziki kila siku na kutapika BONGO FEVER. Hivi mzee Kitime mmekwenda UNDP kama nilivyoshauri? HEbu fanyeni muwe karibu na kufanya bendi ya kudumu. Watanzania wamechoka na miziki kelele ya BONGO FEVER na miziki ya kutajataja majina kutwa kucha ya bendi zinazojiita za dansi kama Twanga Pepeta. Halafu ninyi wazee mtarudisha heshima kwenye game. siku hizi uanamuziki ni uhuni. Yani wanamuziki wa kileo ni kashfa kila kukicha. Hebu okoeni hii tasnia ya mziki jamani isipotee.

    Yani nimekosa uondo kwa kuwa nje ya nchi. Kama Komandoo Kalala na Mzee Mabera walikuwepo nani alipiga Solo? Nafahamu mchawi wa keyboard Abdul Slvador "father keydevu" alimiliki kinanda. Pengine mzee Bitchuka (nimesoma na mtoto wake Salum) alikuwa sauti ya tatu (tenor). Maalimu Ngurumo pengine alichukua sauti ya pili (alto?). Ya kwanza (soprano) ulichukua wewe Balozi kitime? Najua chipsi alikaanga Baba Diana. Aha we acha tu, ilikuwa utamu mtupu hapo.

    ReplyDelete
  6. Anonymous10:45

    Kusema ukweli ninapoandika mistari hii ninasisimkwa mwili, na kufurahia kile ninachokiona katika taswira ulizotuma John.
    Ninahakika hakuna sentensi sahihi inatakayo weza kutoka kwenye kinywa cha binadamu yoyote mwenye akili timamu, zaidi ya kushukuru kwa kusema ASANTENI SANA WAKONGWE WETU.
    Ninapenda kutoa changamoto kwa makampuni ya tofauti tofauti yanayofanya biashara hapo tanzania kuitumia nafasi hii ya kuwapata wakongwe hawa na kufanya nao maonesho sehemu mbali mbali za Tanzania. Watu kama TBL,Serengeti brew na wengine, wangeweza kuwa na matamasha ama tamasha moja la muzikiwa dans kwa kuwatumia wakongwe hawa. bado kuna kada fulani ya watu ambao wanahitaji starehe na ndio wenye FEDHA.
    Nimekuwa nikitazama taswira katika blog ya JIACHIE na kuona kile nilichokiona ambacho kinaitwa TAMASHA LA FIESTA hapo morogoro.
    Nimesikitika kuona at muziki wa kizazi kipya wakicheza kwa back up ya CD sijui kunaweza kuwa na kizazi gani cha muziki kitakacho bakia.
    Hongereni sana John na wakongwe wenzako na poleni sana watu wa bongo flava na wale waandaaji wa TAMASHA LA FIESTA kwa kushindwa kuona mbali

    ReplyDelete
  7. Anonymous11:38

    Mzee Kitime hii kitu mliyoandaa itakuwa ya kudumu au itakuwa kila baada ya mwaka? Kwa kweli mie binafsi nimeguswa sana ila sikubahatika kuhudhuria nilikuwa na udhuru ila naomba kama itafanyika tena ningependa sana kujua lini na wapi kwa kweli baada yenu kutakuwa hakuna mziki kabisa kabisa.

    ReplyDelete
  8. Kulikuwa na mkutano wa wote walioshiriki, kuna mpango wa kurekodi nyimbo mbili zilizotungwa na kikundi, pia kunaangaliwa uwezekano wa tour ya kundi zima , nia ni kuendeleza taaluma yetu kwa kizazi kipya

    ReplyDelete
  9. Kulikuwa na mkutano wa wote walioshiriki, kuna mpango wa kurekodi nyimbo mbili zilizotungwa na kikundi, pia kunaangaliwa uwezekano wa tour ya kundi zima , nia ni kuendeleza taaluma yetu kwa kizazi kipya

    ReplyDelete
  10. Kulikuwa na mkutano wa wote walioshiriki, kuna mpango wa kurekodi nyimbo mbili zilizotungwa na kikundi, pia kunaangaliwa uwezekano wa tour ya kundi zima , nia ni kuendeleza taaluma yetu kwa kizazi kipya

    ReplyDelete
  11. juzi wakati akifunga bunge, president aliwafagilia akina bongo fleva. nadhani alipitiwa kidogo kuwa 'mambo iko huku' kwenye muziki wa dansi.

    ReplyDelete
  12. juzi wakati akifunga bunge, president aliwafagilia akina bongo fleva. nadhani alipitiwa kidogo kuwa 'mambo iko huku' kwenye muziki wa dansi.

    ReplyDelete

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...