YOUTUBE PLAYLIST

Sunday, February 7, 2010

Wanamuziki kutoka Kongo


Huwezi kuongea kuhusu muziki wa bendi Tanzania bila kutaja wanamuziki kutoka Kongo. Kuna sababu kadha wa kadha. Kwanza historia. 1945 kwa sababu za kipropaganda Wamarikani walianzisha kituo cha radio kikubwa katika mji unaoitwa sasa Kinshasa hii iliwezesha muziki wa Wakongo kusikika katika eneo kubwa la Afrika ya kati na mashariki, 1947 ndugu wawili wa Kigiriki walianzisha record company katika mji unaoitwa sasa Kinshasa na santuri za wanamuziki kama Wendo Kolosay na nyimbo kama Akili ya bibi sawasawa mtoto mdogo zilisambazwa chini ya label ya Ngoma na Loningisa na kusambaa sana nchini kwetu, mambo haya mawili yaliweza kuusambaza muziki wa Kikongo katika maeneo yaliyoizunguka na kufanya wanamuziki kuanza kuiga mipigo ya Wakongo. Vita ya wenyewe kwa wenyewe ilianzisha kuhama kwa wanamuziki kutoka Kongo na kuja Afrika Mashariki. Kati ya wanamuziki wa kwanza kuja huku ni Paschal Onema. Lakini baada ya hapo zilikuja Bendi nyingi. Nakumbuka Super Bocca na wimbo wao Suzana mwana Tanzanie, Maquiz du Zaire, Fauvette haya jamani karibu tuendelee .........Pichani ni Mzee Makassy mara tu baada ya kuingia nchini kutoka Uganda

Enzi za Buggy

Katika miaka ya 60 hadi katikati ya 70 kulikuwa na bendi nyingi za vijana ambazo unaweza kulinganisha na wanamuziki wa sasa wanaojulikana kama kizazi kipya. Katika jiji la Dar es Salaam, kulikuweko na bendi nyingi kama vile The Sparks, The Comets, The Flames, The Jets, Crimson Rage, The Lovebugs, Trippers Imagination, Safari Trippers, Afro 70. je unakumbuka nyingine ?

Bendi Zetu

Tanzania tuna bahati mbaya ya kutokuweka kumbukumbu nyingi sana. Kati ya hizo ni kumbukumbu za bendi gani au vikundi gani vya muziki viliwahi kuweko. Labda tusaidiane kila mmoja wetu ajaribu kukumbuka ni kikundi gani kilikuweko wilayani kwake nianzae na mifano michache
******
Iringa-
Highland Stars
Tancut Almasi Orchestra
Chikwala chikwala
Ruaha International
Vico Stars
Mkwawa Orchestra
******

Morogoro
La Paloma Jazz
Cuban Marimba
Morogoro Jazz
Les Cubano
Vina vina Orchestra
******

Ifakara
Sukari Jazz
Kilombelo Jazz
Malinyi Jazz
Kwiro Jazz
Mahenge Jazz
******

Tanga
New Star Jazz
Jamuhuri Jazz
Atomic Jazz
Tanga International
Amboni Jazz
******

Tabora
Tabora Jazz
Nyanyembe Jazz
Kiko Kids haya tuendelee
******

Mwanza
Orchestra Super Veya
******

Moshi
Orchestra Zaire Success
Bana Africa Kituli
********

Mpwapwa
Mpwapwa Jazz
******

Dodoma Jazz
Dodoma International
Materu Stars
Saki Band
Super Melody
*****

Songea
Tembo Jazz
Orchestra Sere sere
******

Lindi
Mitonga Jazz
******

Masasi
Kochoko Jazz

Saturday, February 6, 2010

Mzee Humplick aliwahi kupigwa marufuku

Je unajua kuwa Mzee Frank Humplick ambaye ndiye mtunzi wa nyimbo kama Chaupele Mpenzi, Embe dodo imelala mchangani, aliwahi kutunga nyimbo iliyopigwa marufuku na kusakwa nyumba hadi nyumba ili kusibakie hata nakala ya wimbo huo? Maneno ya wimbo huo yalisema hivi:
Uganda
nayo iende

Tanganyika ikichangaruka, Kenya na Nyasa zitaumana

Nasikia fununu wanavyoichanachana China, Kitisho!

I am a democrat, I don't want communism, English, Yes, No I don't know, Kizungu sikijui

Wanyika msishindane na Watanganyika

Wimbo huo ukaanza kutumika kabla ya mikutano ya Mwalimu Nyerere na kuanza kuwa maarufu kama wimbo wa kudai uhuru, wakoloni haraka sana wakaona wimbo huu utaweza kusababisha vurugu kama ambazo zilikuwa zinaendelea Kenya chini ya Maumau. Serikali ikaupiga marufuku na kuanza kuusaka nyumba hadi nyumba

Friday, February 5, 2010

Young Audiences Music Award

2 February 2010, Jeunesses Musicales International (JMI) launches a call for nominations for the Young Audiences Music Award 2010, an international prize that will celebrate top musical productions for children and youth.

"Looking at the quality of productions presented in schools and within education and audience development programs today, it's obvious that a new standard has been set" said JMI Secretary General Blasko Smilevski "What we see are productions nothing short of spectacular - in terms of artistry but also in terms of message. The once common ‘What instrument is this? lesson' is being fast replaced by subtle teachings on social, environmental, and intercultural issues through music."

Do you know a young audiences production with impact? Visit the all-new www.yama-award.com to apply today! Deadline for submissions is May 1st 2010, thereafter an international panel of experts will select 5 finalists to be presented online and open for public vote. The best productions, one selected by the expert panel and the other by public vote, will win €2,500 each, towards a future production for young people and children. The winners will be revealed at the Young Audiences Music Award ceremony to take place in Skanderborg, Denmark in October 2010.

The Young Audiences Music Award aims to identify and support cutting-edge productions that impact young people with both social and artistic value, targeting and engaging vulnerable/at-risk groups of youth from marginalized communities and deprived areas, addressing issues of vital concern (eg. violence, poverty, discrimination, abuse, HIV/AIDS) and that use music as a tool to promote intercultural dialogue and understanding. All of JMI's work with young audiences is based on the underlying principal that all children and youth should receive access to music/culture as a fundamental human right. Thus, although in many nations we now celebrate an improvement in the music programs of education institutions, the YAMA serves as a beacon of hope to those still facing less than desirable circumstances, to continue the fight for this crucial sector of human development.

YAMA is a JMI Young Audiences Working Group Initiative

More info:

Matt Clark
Communications Officer
Jeunesses Musicales International
matt@jmi.net

T. +32 2 513 97 74

Jeunesses Musicales International (JMI) is the world's largest youth-music NGO. With a mission "to enable young people to develop through music across all boundaries," JMI reaches over 5 million young people aged 13-30 annually through 36,000 activities and is the leading organization in the field of young audiences.


Thursday, February 4, 2010

Mara nyingine mtu unaweza kuanza kupata picha kama vile wanamuziki wako Dar es Salaam tu, jambo ambalo si kweli. Japo ukweli ni kuwa zamani kulikuweko na Bendi karibu kila wilaya nchini. Hapa ni bendi 2 kutoka Dodoma. Super Melody na Saki Stars.
Mwenye gitaa na jaketi la rangi mbili ni Mzee Ikunji, huyu pamoja na kupigia bendi kama Tabora Jazz pia alikuweko Tancut Almasi Orchestra na ndie aliyepiga second solo kwenye nyimbo kama Masafa Marefu, Nimemkaribisha nyoka, na Kashasha

Hii ni Bendi inayoitwa Karafuu Band,moja ya bendi kadha wa kadha zilizo na masikani Zanzibar. Mwenye miwani ya jua ndio kiongozi wa bendi anaitwa Anania Ngoliga, ni mwanamuziki mwenye ulemavu wa macho lakini kati ya wanamuziki mahiri Tanzania. Anania ambaye kwa wakati huu yuko Marekani katika tour ambayo anasindikizana na mwanamuziki Bela Fleck. Fleck amepata grammy awards 3 mwaka huu. Na katika album iliyopata awards kuna nyimbo 2 ambazo zimetungwa na Anania. Anania kisha kuwa mwanamuziki katika bendi ya Legho Stars, Afrisongoma, Tango Stars, Tacosode Band. Amesharekodi na wanamuziki wengi mahiri wakimataifa akiwemo Kriss Kristoffeson, na Zapmama

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...