YOUTUBE PLAYLIST

Tuesday, December 15, 2009

wanamuziki wa tanzania


Nadhani kuna haja ya kueleza muziki na wanamuziki wa Tanzania kiukweli, na si kwa ajili ya promosheni au kwa ajili ya kusifia au kuponda kama mpenzi au shabiki wa muziki bali kavu kavu.Tanzania nchi kubwa yenye watu zaidi ya milioni 35, ina makabila zaidi ya mia moja kumi na tano, ina muziki wa aina nyingi sana. Bahati mbaya kwa wanamuziki , muziki , Watanzania, na ulimwengu kwa ujumla, wale wachache ambao wanauwezo wa kuweka hadharani hazina hii kubwa ya muziki hawana habari wala shida ya asilimia zaidi ya tisini ya muziki wa Tanzania.

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...