YOUTUBE PLAYLIST
Thursday, February 28, 2013
Friday, February 18, 2011
Super Kamanyola ya Mwanza
Beno Villa Anthony |
Beno |
Mukumbule Parash |
Super Kamanyola |
Ally Yahaya na Roy Mukuna |
Beno na Parash |
Anna Mwaole |
John Hamisi |
Sunday, October 10, 2010
WANAMUZIKI WA TANZANIA
Friday, October 8, 2010
The Upanga Story - The Strokers
The Strokers, hili lilikuwa kundi jingine la wanamuziki wa Upanga. The Strokers lilikuwa na awamu mbili, ya kwanza ilikuwa na wanamuziki akina Donald Max, David Max, Harry Chopeta, Vincet Chopeta, Pino Makame na Ochiwa na Freddy Lukindo. Awamu ya pili ya kundi hili ilikuwa na Sajula Lukindo,Onesmo Kibira,Innocent Galinoma,Ben Galinoma, Denis Pad,Francis Kasambala,Vicent na Harry Chopeta, Ally Mwarabu, Sabri Mmanga na wengineo. Pichani ni awamu ya kwanza ya Strokers. Waliosimama, Pino Makame, Freddie Lukindo, David Max. Waliokaa (?),Harry Chopeta, Vincet Chotepa.
Thursday, October 7, 2010
Upanga Story extra
Thursday, September 30, 2010
Sikujua kama utabadilika - Simba wa Nyika
Wengi tunaufahamu wimbo Sikujua Kama Utabadilika, wenye maneno yafuatayo....
Ohhh Sikujua kama utabadilika
Ohhh Ulimwengu kweli una mambo mengi
Baki salama oo kuonana nawe ni majaliwa
Chorus
Utalia utalia ooo usinione, Mombasa mbali, Kakamega mbaali......................
Wimbo huu ulitungwa na Wilson Peter kama kijembe, baada ya mpiga rythm wa Simba Wa Nyika, Prof. Omar Shaaban kwenye mwaka 1978 kuondoka na karibu kundi zima la Simba wa Nyika na kwenda kuanzisha Les Wanyika ambao nao waliokuja na vibao vikali sana katika album yao ya Sina Makosa.
Tuesday, September 28, 2010
Western Jazz Band 2 (Rashid Hanzuruni)
Rashid Hanzuruni, kama ilivyo watu wote walio mahiri katika vyombo vyao vya muziki alilipenda gitaa lake na alifanya mazoezi kila alipopata muda. Kwa maelezo ya mtu aliyekuwa karibu nae alisema huyu bwana kuna wakati dansi likisha isha watu wanaenda kulala yeye aliwasha tena mashine na kuanza mazoezi ya gitaa. Kuna hadithi ambayo hata mimi niliiamini kwa miaka mingi kuwa Doctor Nico alipokuja Tanzania alimuulizia Hanzuruni, hadithi hii si ya kweli. Kwa malezo ya mtu aliyekuweko kipindi hicho, Western Jazz walialikwa kupiga pamoja na Dr Nico alipokuja Tanzania kati ya mwaka 66 na 67, na katika maonyesho hayo, kwanza Hanzuruni ndipo alipomuona Dr Nico kwa karibu na kupenda staili ya upigaji wake, na pia ndipo alipomuona Dr Nico akipiga Hawaian Guitar, nae akalipenda na Western Jazz wakalinunua na Hanzuruni akawa mpigaji wa kwanza Mtanzania wa gitaa la hawaian,baada ya hapo Hanzuruni alifanya sana mazoezi ili aweze kupiga gitaa kama Dr Nico. Ni vizuri kulisema hapa kuwa Hanzuruni ndie alikuwa mwanamuziki aliyelipwa vizuri kuliko mwanamuziki yoyote wa Dar Es Salaam wa aina yake, katika kipindi hicho.
SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...
-
Hawa ndio The Jets (1972), ambao baadae walikuja kuwa STC Jazz, ambayo ndio chanzo cha Biashara Jazz. Waliopo hapa wa kwanza Belino, Raphael...
-
Mara baada ya kutoa ule wimbo maarufu wa Kisambaa Shakaza, Eddy Sheggy mwenyewe na Wasambaa wengine wakaanza kuitwa Shakaza. Eddy Sheggy ali...
-
Suleiman Mbwembwe, aliyekuwa anajulikana pia kwa jina la Electronic Voice, alikuwa mwimbaji na mtunzi aliyeng'ara katika enzi zake. Aki...