YOUTUBE PLAYLIST

Tuesday, February 2, 2010


Hii ni label ya santuri mojawapo ya zamani. Katika miaka hii kulikuwa hakuna wizi wa kazi za sanaa kama ilivyo sasa. Teknolijia ilikuwa haiwezeshi mtu kukaa chumbani kwake na kunakili kazi za watu

Monday, February 1, 2010

Two generations

Huwa nafurahi kila nikipata chance ya kuona show ya Shaa u r great girl

Matangazo ya Bendi zamani yalikuwa yakipambwa na vituko mbalimbali. Wakati huo matangazo yalikuwa yakitoka katika magazeti tu. Na magazeti yalikuwa hayana teknolojia ya kutoa picha za rangi. Hili ni tangazo la bendi ya Maquis ambayo kwa wakati huo ilikuwa na wanamuziki karibu hamsini

Tulikuweko tupo tutakuweko


Enzi za ujana si mwingine ni Dr Remmy Ongala wakati huu akiwa na Orchestra Makassy

Tulikuweko tupo tutakuweko


Miaka hiyooo staili hii iliitwa bumping. ilianza hasa baada ya wimbo ulioitwa Kung Fu fighting. Hapa ni Marehemu Mbaraka Mwinyshehe akiwa Songea wakati huo na Morogoro Jazz Band

Album Throw down your heart ambayo ndani yake kuna nyimbo kadhaa ambazo amepiga mwanamuziki Anania Ngoliga imeshinda grammy awards

Wasanii ni kioo cha jamii, huu ni usemi ambao umezoeleka sana siku hizi katika vyombo vya habari na hata baina ya wasanii wenyewe. Usemi huu niliusikia kwa mara ya kwanza kutoka katika kinywa cha moja ya wasanii mahili nchini marehemu Mzee Godfrey Kaduma, ambaye pamoja na kuwa msanii mahiri ambaye kumbukumbu za usanii wake zinapatikana katika maandishi mengi na filamu kama vile Harusi ya Mariamu. Mzee Kaduma alieleza wazi kuwa usemi huo ni tafsiri ya usemi wa kiingereza ,”Artists are the mirror of the society”. Mirror ni kile kioo ambacho unajitizama ujione ukoje. Hivyo basi jamii ya Kitanzania ikitaka ijijue ikoje iwaangalie wasanii na kazi zao na ijue inajiangalia yenyewe. Msanii asie itafsiri jamii yake hujikuta yuko peke yake hana wapenzi.

Katika miezi miwili iliyopita kumejirudia jambo ambalo kila mara mimi huliona la ajabu sana. Na hii ni tabia ya viongozi kupiga marufuku shughuli fulani za kisanii. Nimesoma katika mikoa miwili wakuu wa mikoa wamepiga marufuku shughuli za kisanii. Kupiga marufuku ni jambo rahisi sana, tena rahisi zaidi katika sanaa kwani wasanii hawajawa na tabia ya kudai haki zao kisheria zinapopigwa marufuku, hivyo viongozi hutoa matamko ya namna hiyo bila woga wa kupata athari za matokeo ya matamko yao.

Tasisi moja imetangaza iko katika mchakato wa kutunga sheria ya kuwabana watunzi wa filamu kuhakikisha wanapeleka tungo zao kuhakikiwa kabla ya kuzitoa hadharani kwani nyingine zinakiuka maadili yetu.

Ningependa kuwakumbusha viongozi wanaopiga marufuku na hawa wanaotunga sheria za kubana watunzi kuwa wakumbuke, wasanii ni kioo cha jamii kwa hiyo yote yanayoendelea katika sanaa yanaonyesha jamii ilivyo. Hivyo basi kuvunja kioo, au kukataa kutumia kioo si njia ya kubadili ubaya wa sura yako.

Tatizo si wasanii, kwani wao ni sehemu tu ya jamii, tatizo ni mmomonyoko wa maadili katika jamii. Wakati unaruhusu vyombo vingine vionyeshe filamu zenye maadili ya kimagharibi masaa ishirini na nne na hivyo kutengeneza jamii inayokubali hayo, halafu kumkataza msanii wa Kitanzania asitunge hadithi ikiwa na maadili hayo mapya, atapata wapi wateja wa kazi zake? Atakachotengeza ataambiwa kazi zako zimepitwa na wakati.

Hata katika nchi ambazo zimeendelea kuna mfumo ambao hutengenezwa kulinda na kuendeleza maadili ya nchi hivyo wananchi kuishi wakiwa wana aina ya maadili ya nchi husika. Vyombo vya kurusha matangazo katika nchi nyingi huwa na asilimia iliyopangwa ya matangazo ambayo huitwa local content. Mfano kama mtu anataka kuendesha Radio au TV anajua kuwa asilimia sitini ya matangazo yake lazima yawe ni kutoka nchini, filamu, muziki na kadhalika, muziki hapa si bongo fleva na muziki wa dansi tu bali hata ngoma za kiasili. Jambo hili ni muhimu sana katika kujenga uzalendo lakini linajenga upenzi wa soko la kazi za sanaa za nchini, na hii inatengeneza ubunifu zaidi katika kazi za sanaa za nchi.

Wakati Balozi wa Japan anaweza akatoa DVD za bure zirushwe katika vituo vya TV nchini ambazo zinaonyesha utamaduni na maadili asili ya Japan, nabaki nawaza Balozi wetu yoyote yule atatoa nini kwenye nchi aliyoko akiambiwa nae atoe filamu toka kwao.

Serikali imeachia utamaduni unaendeshwa na wafanya biashara, matamasha mashindano , kutafuta vipaji na kadhalika kwa misingi ya biashara unafanya kitu kinacholipa. Serikali iwekeze tena kama zamani katika sekata hii ili kuweza kufufua na kukuza utamaduni wa Mtanzania ambao sasa unakokwenda ndio tunaonyeshwa na wasanii ambao kwa kuwazuia haisaidii kubadili mwelekeo wa maadili ya watu.

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...