YOUTUBE PLAYLIST

Saturday, August 13, 2022

NGOMA AFRICA BAND KUTIKISA KWENYE TAMASHA LA KIMATAIFA LA AFRIKA EXPO, TUBINGEN,GERMANY 2022


BENDI  maarufu ya  Ngoma Africa band itashiriki katika burudani za kukata na shoka zitakazotumbuiza wahudhuriaji wa tamasha  la  15 la International African EXPO  Festival  litakalofanyikaTübingen, Ujerumani. Tamasha litakuwa kati ya tarehe 01September - 04th September 2022  Fest Platz,  Tübingen, Ujerumani.
Ngoma africa band watakuwa jukwaani Jumamosi 03 September 2022
Ngoma Africa, ni bendi yenye makao yake Ujerumani na ilianzishwa mwaka  1993 na kiongozi wa bendi hiyo Ebrahim Makunja anaejulikana pia kama Kamanda Ras Makunja. Bendi hii ina wanamuziki wakali kama soloist Christian Bakotessa aka Chris-B, wengine ni Jo Souza, Matondo Benda, Aj Nbongo, Flora William, Jessicha Ouyah, Vially Nbongo, na wengio. Bendi hii ina mamilioni ya wapenzi na inajulikana kwa kupagawisha kwa midundo yake yenye uasili wa Afrika ya Mashariki.

Ngoma Africa imeshaachia CD kadhaa ikiwemo CD yake mpya inayoitwa “BONGO TAMBARARE” , nyimbo mbili hizi  "Mapenzi ya Pesa" na "Supu Ya Mawe" unaweza kuzisikiliza ukiingia hapa www.reverbnation.com/ngomaafricaband

No comments:

Post a Comment

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...