YOUTUBE PLAYLIST

Sunday, April 2, 2017

TUMETIMIZA MIAKA 11 TOKA KUONDOKEWA NA TX MOSHI WILLIAM


Mazoezini katika ukumbi wa Amana katika uhai wake
Moshi William alizaliwa mwaka 1958 hale Mwakinyumbi Korogwe. Pale palikuwa na Mzee mwanamuziki maarufu aliyekuwa akiitwa Mzee Masongi na bendi yake ilikuwa chnzo cha wanamuziki wengi maarufu akiwemo Moshi William. Jina halisi la Moshi William lilikuwa Shaaban Ally Mhoja lakini alikuja kubadili na kuitwa Moshi William kutokana na kuja kulelewa na baba mwingine. Alipewa kisifa cha TX, na Julius Nyaisanga.

Moshi alifariki siku ya tarehe 29 March 2006 katika wodi ya Sewa Haji baada ya operesheni ya kuondoa chuma katika mguu wake uliovunjika kwenye ajali. Alifariki saa tatu kasoro robo asubuhi na kuzikwa siku hiyohiyo katika makaburi ya Keko Machungwa. Moshi lipitia bendi kadhaa baada ya kutoka Hale zikiwemo UDA Jazz, Safari Trippers, Polisi Jazz na hatimae kutua JUWATA 1982. Ambapo aliweza kutuacha na album 13. Na pia alishinda tuzo la mtunzi bora kuanzia mwaka 2003 hadi 2005.
Kaburi la Moshi William

Mungu amlaze pema Shaaban Ally Manongi, TX Moshi William

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...