YOUTUBE PLAYLIST
Monday, July 5, 2010
Orchestra Mambo Bado
Orchestra Mambo Bado ilikuwa bendi ambayo haikukaa kwa muda mrefu katika anga za muziki. Bendi hii ilianza mwaka 1981, ikiwa chini ya 'Mtoto Mzuri' Tchimanga Assossa ikajulikana sana kwa ajili na mtindo wake ulioitwa Bomoa Tutajenga kesho. Pichani Sadi Mnala Drums (yuko Msondo), William Maselenge rythm guitar(marehemu), Andre Milongo(?), Bass na Second Solo, Kazembe wa Kazembe(marehemu) Solo guitar. Pamoja nao walikuweko John Kitime(Njenje), Jenipher Ndesile (?), George Mzee(Marehemu), Likisi Matola(Moonlight Band),Lucas Faustin(Police Brass Band) na Huluka Uvuruge(Msondo), baadae Athumani Cholilo(Marehemu) na Banza Tax(Marehemu), Selemani Nyanga(Uholanzi), Nana Njige(Marehemu). Wimbo wao Bomoa Tutajenga Kesho ulipigwa marufuku.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.
TANCUT ALMASI ORCHESTRA wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...
-
Hawa ndio The Jets (1972), ambao baadae walikuja kuwa STC Jazz, ambayo ndio chanzo cha Biashara Jazz. Waliopo hapa wa kwanza Belino, Raphael...
-
Mara baada ya kutoa ule wimbo maarufu wa Kisambaa Shakaza, Eddy Sheggy mwenyewe na Wasambaa wengine wakaanza kuitwa Shakaza. Eddy Sheggy ali...
-
Suleiman Mbwembwe, aliyekuwa anajulikana pia kwa jina la Electronic Voice, alikuwa mwimbaji na mtunzi aliyeng'ara katika enzi zake. Aki...
Asante sana mzee Mwakitime, siku-note kama nawe ulikuwemo kikosini, bravo kaka. Hii bendi ilidumu muda mfupi lakini ilikuwa na vibao moto sana. Umenifanya nimkumbuke tena marehemu Nana Njige kwa kweli huyu dada alikuwa ni unique kama Kida Waziri kwa sauti zao zinazojipambanua. Umenikumbusha kibao "Ilikuwa jambo dogo, Ilikuwa jambo dogo tu mama, mitaani kote limeshaeneaa jamaaa...angalia sasaa...angalia sasaa umeshazeeka".
ReplyDeleteSauti ya Nana hapo ilichombezea kwa raha tamu inayopita sikioni hadi moyoni
Sie ndo tulikuwa wanzilishi, tukiwa na nyimbo kama Bomoa tutajenga kesho,mawazo, kutokuelewana, wakati huo mwimbaji wa kike alikuwa Jenifa Ndesile
ReplyDeleteKitime shukrani sana kutukumbusha Orch.Mambo Bado na hongera sana kwa Tshimanga Assosa kwa vile anazidi kulisukuma libeneke(Bana Maquiz).
ReplyDeleteBendi karibu ya Mwisho ambayo mpiga solo Kazembe wa Kazembe alikua nayo kabla hajatangulia kwa Mola ilikua Chamwino Stars alikua akishirikiana na Dekula Kahanga(Vumbi)na makao makuu yao ilikua pale Tandale...kiisha Kazembe kachukuliwa na Wafaransa fulani...Dekula Kahanga naye kachukuliwa na Maquis hapo ilikua mwaka 1985
Sakubaa, sakuba sakuba - mambo ya siku hizi
ReplyDeleteDiscoee, Disco agwaya
Wew acha tu
Mdau hapo juu, hicho kilikuwa ni kionjo cha Orchestra Makassy, sio Mamba Bado. Makassy hiyo ilikuwa ni enzi za akina Assosa na Maliki Star.
ReplyDelete