YOUTUBE PLAYLIST

Tuesday, May 4, 2010

Wanamuziki ndugu


Katika kila nyakati kunatokea ndugu ambao ni wanamuziki. Pengine hii inatokea kwa kuwa mtu anakulia katika mazingira ya nduguze kupiga muziki hivyo inakuwa rahisi kwake kuwa mwanamuziki, na nduguze wakiwa wanamuziki inamrahisishia njia, lakini hilo si jibu sahihi kwa kweli kuna mengi zaidi ya hilo. Katika picha hii ni wanamuziki ambao ukoo wao wako wanamuziki wengi na hii imekuwa inaendelea kwa vizazi vitatu sasa jina la ukoo huu kila mara likiwemo katika historia ya muziki. Ni akina nani hawa?

34 comments:

  1. Kwa kweli nitahisi tuuu. Kwa kuwa nimeona gitaa, ntasema ni kina UVURUGE.
    Just guessing

    ReplyDelete
  2. Hapana , kumbuka nimesema katika ukoo huu kumekuwa na historia ya muziki ambayo imekuwa katika kizazi zaidi ya kimoja

    ReplyDelete
  3. Anonymous10:27

    Me too, just guessing (they look too young): Kina Mhuto???

    ReplyDelete
  4. Picha ya miaka ya mwanzo mwa 70s

    ReplyDelete
  5. Anonymous23:14

    Kina Issa Juma wale ndugu ambao walikuwa Les Wanyika?

    ReplyDelete
  6. Anonymous23:14

    Lakini siyo Marijan Rajab na kaka zake hawa?

    ReplyDelete
  7. Anonymous15:34

    Balozi John,
    hawa nimeshindwa kabisa kuwajuwa ingawaje nilikuwa mmojawapo wa wapenda mziki tokea mwishoni 69 mpaka mwishoni 70`s hawa vijana wanaonekana walikuwa wadogo sana,
    tupe mwelekeo kidogo labda utasaidia,walikuwa wanaishi wapi tutajaribu kupata mwanzo wa kuwakumbuka hawa siyo kabisa kina mhuto,sabuni au barkeys.
    Mickey Jones
    Denmark

    ReplyDelete
  8. Nasubiri "kutoa mji". Hahahahaaaaaaaaaaaaa

    ReplyDelete
  9. Bado sitaki mji clues zote nimezitoa, ukoo wao washiriki wa music wameingia generation ya 3

    ReplyDelete
  10. Anonymous01:28

    Huu ni ukoo wa mwinshehe na hiyo picha ni yeye hapo

    ReplyDelete
  11. Anonymous19:05

    ukoo wa kina Mze Zahir Ally Zoro

    ReplyDelete
  12. Ngoja nitoe clue nyingine. Group hii ilikuwa inaitwa The Gypsies, ilitokana na kaka zao kuwa na bendi iliyoitwa Les Heroes. Mpigaji mmoja wa Les Heroes bado anapiga na ana mwanae ni mwana muziki

    ReplyDelete
  13. Anonymous19:46

    Dk John,

    Umenichanganya kabisa nawakumbuka Les Heroes nawakumbuka The Gypsies, lakini kila nikizungurusha ubongo kupata kumbukumbu nazungurusha kichwa kizima bila ya kupata jibu.
    Dares salaam upande wa magomeni kulikuwa na The Comets na kina mhuto`s, Les Heroes na Mohamed Makwinyo,Gabriel Sabuni,Gershom Chihota,Abby Sykes upanga kulikuwepo na sasa mhs. Mohamed Maharage(James Brown)willy Lukuta na The Groove Makkers,kulikuwepo Barkeys,changombe kulikuwepo na Mussa Gordon,Shabani Marijani na Les Trippers,Temeke kulikuwepo na Patric Balisidya na Afro 70,James, Kassim na The Sun Burst sasa hawa vijana jipukizi nakumbuka walipiga ma-gigi wakati wa mapumziko sehemu nyingi nilizokuwepo kama Splendid hotel,Karmjee Hall na secondary schools zote kama St Josephs sasa forodhani...nimekwama siwakumbuki, nimetuma maombi ya msaada kwa mshikaji wangu Freddy Macha wa 70`s hajanijibu nafikiri hata yeye kakwama hawakumbuki..
    Nafuatilizia lazima zawadi iwepo kwa mwenye kumbukumbu ya vijana.

    Mickey Jones
    Denmark

    ReplyDelete
  14. Baba yao aliishi Temeke

    ReplyDelete
  15. Anonymous01:08

    ukoo wa sykes,kwa sasa anayetamba ni dully sykes(abdul)

    ReplyDelete
  16. Anonymous14:30

    Hii ya safari hii ni chemsha bongo. Mimi late 60's na early 70's nilikuwa nakwenda boogie na nilibahatika kufahamiana na wanamuziki wengi, k.m. kina Sabuni, marehemu Adam Kingui, marehemu Balisidya, Mick Jagger, Salim, Sunbursts, etc, na the Heroes. Cha ajabu hii picha doesn't ring a bell in my mind. Au huu ndio uzee??? Hapa ni case ya kuomba "msaada tutani". Eddy.

    ReplyDelete
  17. Anonymous14:36

    Kama asemavyo mchangiaji kuwa ni ukoo wa Sykes ambaye mtoto wake ni Dully Sykes, basi atakuwa Abby sykes wa Les Heroes akiwa pamoja na Mohamed Makwinyo,Gabriel Sabuni,Gershom Chihota na Choggy Sly rafiki au kundi langu la ujana 70`s.
    Abby Sykes hakuwa mkaaji wa Temeke zaidi ya kuwatembelea jamaa na marafiki zake kama mmojawapo wakati huo alikuwepo jirani yangu marehemu Abushiri Kilungo,kina Sykes waliishi mitaa Ilala karibu na John Rupia,wakati ule kulikuwepo na The Rifters/Sparks mwimbaji alikuwa Ringo Star mpiga drums maarufu jina nikikumbuka alikuwa Mbaraka,jirani kulikuwepo kijana mwimbaji chipukizi wa The Comets akiitwa Huruka (HULKY) kina Sykes wengine walikuwepo upanga na magomeni.
    Nimepoteza kumbukumbu,tuendelee kuwasikiliza wenye kumbukumbu za hawa vijana

    Mickey jones

    ReplyDelete
  18. Anonymous20:12

    Brother John
    Huyu ni Omari Sykes, mdogo wake Adam na Ebby Sykes, Ebby ni baba yake Dully Sykes
    Balozi Maharage Juma

    ReplyDelete
  19. Anonymous20:22

    Hi Mickey Jones yaani umemsahau marehemu Omar Sykes? Ndiye huyo pichani!Habari za Denmark?
    Balozi Mohamed Maharage Juma, tuwasiliane kwnye mabeans@gmail.com

    ReplyDelete
  20. Mheshmiwa Balozi welcome. niseme nini? I got soul and I am super bad.

    ReplyDelete
  21. Anonymous22:46

    Ahsante brother John unanikumbusha mbali sana nategemea kuwepo home July nasikia Njnje inatayarisha usiku wa vijana wa zamani tupande jukwaani!
    Mohamed Maharage Juma

    ReplyDelete
  22. Anonymous15:59

    Karibu balozi ukumbini kwa kaka John Mwakitime,pongezi zote kwa kuturudisha miaka iliyopita.

    Balozi nimeshapata habari hizo za July lazima niwepo nyumbani sitokosekana ratiba hiyo ya usiku wa vijana.

    Nilipigiwa simu na waziri Mahanga wakiwa pamoja na balozi Cisco,pia nilipata bahati mara mbili kukutana na mhs Rose Migiro wote niliwaomba wapitishe salaam zangu kwako haswa wakati wa kifo cha marehemu mtoto.ahsante kwa kumbu kumbu za mtoto wetu Omary Sykes

    Mickey Jones

    ReplyDelete
  23. Anonymous09:56

    Ahsante Mh. M.M.Juma. Kweli huyo ni Marehemu Omari Sykes. Hii picha imenikumbusha mbali na kunipa huzuni, lakini kazi ya Muumba haina makosa. Tunamwomba Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peoni. Amin.
    Eddy.

    ReplyDelete
  24. Anonymous03:55

    Yep, Balozi Maharage is right, huyo ni Omari Sykes(RIP) was a good friend of my brother Andrew(RIP). Good to see you are in circulation. I guess you could consider me a groopie of the "Groove Makers" back then I attended all theeir "Boogies" As far as I am concerned together with my good friend and classmate Herbert Lukindo(RIP), the Jengo brothers, Sverne Kibira, you guys were the best

    Sammy Mnkande

    ReplyDelete
  25. Anonymous12:07

    Very sad to hear that Herbert Lukindo has passed away. May he rest in peace. Amin.

    ReplyDelete
  26. Anonymous12:07

    Very sad to hear that Herbert Lukindo has passed away. May he rest in peace. Amin.

    ReplyDelete
  27. Anonymous13:56

    Hi Sammy..
    kweli umenikumbusha mbali,ilikuwa hakuna "gigi/buggy" watakalopiga The Groove Makkers ukawakosa kina Jengo brothers,kibira,Anne Mkande,Makame wa Upanga na R.I.P Herbert Lukindo ambaye alikuwa na uhusiano na Willy Lukuta mpiga bass....
    Mickey Jones

    ReplyDelete
  28. Anonymous14:10

    R.I.P Herbert Lukindo
    yes...very sad,sote tulishikwa na majonzi makubwa kutoweka kwa rafiki Herbert Lukindo alikuwa "Gentle & Cool" mara ya mwisho mimi kumuona aliporudi toka China,tulienda kwake na Willy Lukuta wa The Groove Makkers.
    Mickey Jones

    ReplyDelete
  29. Anonymous20:16

    Hi Sammy
    Nice to know you are in circulation too, pia tumkumbuke rafiki yetu mwingine marehemu Hamis Mapezi mlikua naye Saint Josephs alikuwa hakosi Buggy!
    MMJ

    ReplyDelete
  30. Anonymous00:24

    mwakitime tunashukuru sana kwa kazi yako nzuri kwa kutuletea habari ya wanamuziki wetu wa zamani na sisi tulioko nje ya nchi tunafaidi sana ubarikiwe sana nilikuwa naomba kama itawezekana utuletee habari ya wale wanamuziki wameamiga arusha long time walikuwa wanajiita kwa jina lombelombe baadhi ya majina yao siwakumbuki wote ila kuna baadhi ya majina msimbe,athumani alikuwa mpiga gitaa lkn marehemu kwa sasa

    ReplyDelete
  31. Nawakumbuka Orchestra Lombelombe, walikuwa ni kundi lililo break away toka kwa Mbaraka, nitatafuta data zaidi nikuletee, najua nina cutting moja ya habari zao ikiwa na picha ya Gumbo ambae alikuwa mpiga bass wao, ntaipost hapa..

    ReplyDelete
  32. Anonymous01:03

    nitashuku sana ukiipost utupostie picha nyinginyingi tu. HAVE A GOOD NIGHT

    ReplyDelete
  33. Anonymous13:20

    Ohhhh my God !!!!
    Hamis Mapezi hatunaye tena....? sikuwa na habari za kutoweka kwake,ametutoka mapema mno,poleni ndugu na marafiki wote wa Hamis.
    balozi MMJ ahsante kwa taarifa
    Mickey Jones

    ReplyDelete
  34. chesi.com19:29


    ...is Anne Mnkande any relation to Lucy Mnkande my classmate at Chang'ombe P/s in 1972/73?

    ReplyDelete

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...