YOUTUBE PLAYLIST

Wednesday, May 12, 2010

Nani hawa? Picha ilipigwa Dodoma 1961


Nimepigiwa simu leo na mzee mmoja akanambia amesikia kuhusu blog hii na ana kitu cha kuchangia. Kanipa picha hii ambayo pengine ni ya zamani kuliko nyingi humu ndani. Kanambia siku moja 1961 alitoroka shule ili aweze kumwona mwanamuziki ambaye alimpenda kuliko wote. Alikuwa anasoma Dodoma wakati huo, na aliweza kupata picha siku hiyo picha hii naiweka kwenu. Swali, nani anaweza kuwataja wanamuziki waliomo katika picha hii.? Wanaoimba hapo wote ni marehemu, anaepiga gitaa yu hai na picha yake ya sasa iko katika blog hii.

8 comments:

  1. Anonymous06:16

    Mkuu,

    Ni Salum Abdallah!

    ReplyDelete
  2. Anonymous10:23

    JM, Huyu ni Marehemu Salim Abdallah (RIP).

    ReplyDelete
  3. Anonymous13:54

    Huyu ni ndiye aliyekuwa nyota wa enzi za mama zetu ni marehemu Salim Abdalah,mwimbaji mwingine simkumbuki,lakini mpiga gita sina uhakika nafikiri ni Dr Ufuta

    Mickey Jones

    ReplyDelete
  4. Anonymous18:33

    Huyu siyo Salim Abdullah?

    ReplyDelete
  5. Anonymous18:57

    Na bendi yake ilikuwa ikiitwa Cuban Marimba Jazz Band. Hawa walikuwa Morogoro. Salim alifariki katika ajali ya gari 1960's kama vile Mbaraka Mwinshehe 1970's. May they rest in peace. Amin.

    ReplyDelete
  6. Najiunga na waliotangulia. Huyo ni Salum Abdallah. R.I.P!

    ReplyDelete
  7. Wanaoimba, kushoto Juma Kilaza na kati Salum Abdallah. Kwenye gitaa Ufuta

    ReplyDelete
  8. Anonymous21:48

    Mkuu,

    Juma Kilaza alifariki lini? Namkumbuka kwa madaha yake na ninakumbuka nyumba yake iliyokuwa imepambwa kama mabasi ya Afghanistani au Vitenge vya kina mama pale mitaa ya Kingo, Morogoro.

    Mwenyezi mungu Amlaze kwa Amani. Amen.

    PS/ Kwenye nyimbo ya Afrika Muye Muye nikiisikiliza kule mwishoni huwa nacheka sana. Kwa yeyote mwenye hiyo nyimbo au CD ya Ngoma Iko Huku tafadhali sikiliza ili tucheke sote mambo ya Marehemu Juma Kilaza ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya jinsi alivyotufurahisha kwa namna anuai.

    ReplyDelete

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...