YOUTUBE PLAYLIST

Wednesday, April 14, 2010

Orchestra Santa Fe

Kati ya maswali amabayo yamewahi kuulizwa humu ni kuhusu bendi hii Orchestra Santa Fe. Hii ilikuwa mwanzo ni bendi yenye asilimia kubwa ya wanamuziki Wakongo. Mkuu wa 'Libeneke' aliwahi kuuliza kama ndio ilikuwa Bendi ya kwanza ya Kikongo, ninauhakika haikuwa bendi ya kwanza ya Kikongo. Wenye taarifa zaidi kuhusu Bendi hii karibuni. Bendi hii ilikuwa ikipiga pale Gateways Mnazi Mmoja maeneo ambayo kuna wakati yalikuwa maeneo muhimu katika shughuli za starehe jijini Dar es Salaam.

2 comments:

  1. BLACKMANNEN03:14

    Orchestra Santa Fe, haikuwa ya Wakongo. Bendi za Fouvette na akina "Papa Mikey" ndiyo waliokuwa Wakongo wa mwanzo Tanzania.

    Orchestra Santa Fe, Tanzania Jazz Band, King Africa Jazz Band na Orchestra Quilado zote zilikuwa za Kitanzania, ila habari zake wengi hatuzijui.

    It's Great To Be Black=Blackmannen

    ReplyDelete
  2. Anonymous23:02

    TP SANTA FE ILIKUWA NI BENDI YA WAKONGO ILINGIA NCHINI IKITOKEA ZAMBIA NA BAADHI YA WANAMUZIKI WA ZAMBIA MMOJA WAPO NI MPIGA BASS JOSEPH MULENGA,WAKATI TP SANTA FE INAPIGA GOROFA YA TANO GATE WAYS SAFARI TRIPPES ILIKUA ATUA CHACHE PRINCESS BAR KUNA SIKU MPIGA BASS WA TRIPPERS MAREHEMU CHRISTIAN KAZINDUKI ALIPATA AJALI YA PIKIKI PALE KONA YA CENTRAL POLICE KUKAWA HAKUNA MPIGA BASS ILIBIDI MASHABIKI TUTOKE KWENDA KUMUZIMA MULENGA ILI DANSI LETU LIPIGWE NANDIO UKAWA MWANZO WA NYOTA YAKE KUNG'AA ALIJIUNGA NA TRIPPERS NA NYIMBO YAKE YA KWANZA KUREKODI MATESO DHIKI NA MATESO AKIPIGA RIDHIM GITAA ,ABDALA GAMA SOLO,BENNY PETTY SECOND SOLO,KAZINDUKI BASS,KABLA YA KUHAMIA DAR INTERNATIONAL NA KUKUTANA NA MZAMBIA MWENZI MKUBWA WAKE MICHAEL ENOCK ALIE MTRAIN KUWA MPIGA SOLO SIKILIZA NYERERE BABA MLEZI NYERERE MWANA MAPINDUZI THEN AKAENDA SIKINDE.

    ReplyDelete

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...