YOUTUBE PLAYLIST

Saturday, April 24, 2010

Maquis Original


Maquis Original wakiwa katika uwanja wa Jamhuri Dodoma. Mwenye nyeusi tupu akiwa na gitaa ni Dekula Kahanga Vumbi, wa pili toka kushoto na suruali nyeusi ni Issa Nundu haya tuwataje wengine hapa.

12 comments:

  1. Anonymous22:11

    BW.KITIME, HAPA NAWAKUMBUKA, L-R: WA KWANZA (IN BLUE) NI MUKUNA WA MUKUNA ROY, WA TATU(IN WHITE) NI MULENGA KALONDJI, HUYU NDIYE ALIKUWA MWANZILISHI NA MMILIKI WA BENDI YA MULE MUVA, WA NNE NI MUTOMBO AUDAX,NA WA TANO NI MUKUMBULE PARASH, HUYU ALIIMBA WIMBO BANGUNGI, NA MWAKA WA WATOTO AKIWA NA BENDI YA KYAURI VOICE...

    ReplyDelete
  2. Anonymous11:17

    Nampongeza sana Vumbi kwa kukumbuka atokako na kuitembelea Tanzania mwaka jana, takriban miaka 18 tangu aondoke nchini na kuhamia Sweden. Natarajia wanamuziki wengine waliowahi kuishi Tanzania kabla ya kutimkia ng'ambo watafuata nyayo zake.

    ReplyDelete
  3. Hata sasa hivi Vumbi yuko Dar anaondoka kurudi Sweden wiki ijayo.

    ReplyDelete
  4. Anonymous11:22

    Kama sikosei hizi zilikuwa ni enzi za 'super sendema' mwaka 1990, baada ya Assosa kuondoka na kujiunga na Legho Stars. Kipindi kifupi baadae kulikuwa na mabadiliko mengine ambapo walikuja watu kama Kivukutu, Freddy Butamu na Bobo Sukari.

    ReplyDelete
  5. Anonymous13:50

    Mdau wa kwanza shukrani kwa kutukumbusha majina ya wana Maquis. Julius Nyaisanga alivyokuwa akiyataja majina ya hawa jamaa kwenye Club Raha Leo Show ilikuwa burudi kwelix2. Kulikuwa kuna Banza Mchafu, nafikiri alikuwa akipiga gitaa la bass kwenye hii bendi.

    ReplyDelete
  6. Anonymous19:08

    HATA KEPI WA NJENJE NAYE ALIPIGA BASS MARQUIS WAKATI FULANI.

    ReplyDelete
  7. Anonymous01:25

    Keppy Kiombile kapigia Maquis 1986-1987,kisha kahamia Afriso Ngoma,ila hakukaa akarudi tena Maquis ndio kachukuliwa na Kilimanjaro...

    Kutoka kushoto ni Roy Mukuna,Issa Nundu,Mutombo Audax,Parash Mukumbule,Kwempa Rissasi,kaumba kalemba.Wapiga Magitaa ni Mulenga Kalonji,Steven Kaingilila na Vumbi Dekula.Drums ni Matei Joseph.Hii ilikua jamuhuri Stadium Dodoma baada ya safari ya pili kutoka Muscat Oman,Maquis ilikua bendi ya kwanza kutoka Tanzania kufungua safari za Oman.

    ReplyDelete
  8. Anonymous04:43

    huyo nyuma mwenye white suti anayepiga gitaa ni nani?

    ReplyDelete
  9. Anonymous10:50

    Huyo mwenye suti nyeupe ni Marehemu Mulenga Kalonji "Vata" mpiga rythm guitar, alikua akimiliki bendi ya Mule Muva katika miaka ya 86 huko Lusaka Zambia baada ya bendi kufa... akarudi tena Maquis 1988

    ReplyDelete
  10. Anonymous19:31

    Huyu wa kwanza kulia ni mmoja wa wale mapacha Kasaloo Kyanga na Kyanga Songa. Mmoja wao nasikia ni marehemu.
    Hongera kaka kwa kutukumbusha muziki wa enzi hizoooooo.

    ReplyDelete
  11. Anonymous02:30

    Huyu wa kwanza kulia ni mpiga Tarumbeta, Marehemu Kaumba Kalemba yeye ndiye katunga Nyimbo ya Makumbele.

    Wale Mapacha,mmoja wao ni Marehemu yaani Kyanga Songa ila Kasaloo Kyanga yuko hai...na bado anaimba katika Bendi fulani Dar-Es-Salaam.

    Kwa kweli tuzidi kumpongeza Mr. John Kitime kwa kazi nzuri anayoifanya...
    Sababu Muziki wa Rumba ao Bongo dance umesaulika Tanzania.
    Vyombo vya Habari havitangazi ipasavyo Muziki huu...

    ReplyDelete
  12. Anonymous11:15

    Habar ni bendi gani imeimba wimbo huu...wewe ndie uliyeanza nilikubembeleza usiku mzima ubadilishe uamuzi wako mama nilijua eee waliokudanganya wako wapi wamekuacha huna pa kuanzia dunia ya leo matata ee oohh miee mamaaeehh

    ReplyDelete

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...