YOUTUBE PLAYLIST

Sunday, April 18, 2010

Enzi za Buggy


Leo ni Jumapili ngoja nilete picha ambayo kwa vyovyote ilipigwa Jumapili , maana ndio ilikuwa siku ya Buggy, lile dansi la mchana lililokuwa linaanza saa 7 au nane na kuisha saa kumi na mbili jioni. Unaona mavazi ya siku hizo?, si muda mrefu baada yalipigwa marufuku , na kukaweko na posters kila mahala zikionyesha nguo gani za kuvaa. Vijana wa TANU Youth League walikuwa wakitembea na mikasi na kuchana nguo zilizoonekana hazifai. Loh, Hawa Rifters walikuwa kati ya makundi mengi ya wanamuziki vijana waliokuwa wakipiga muziki wa soul, hapa bwana nyimbo za Otis Redding, Kipofu Clarence Carter, Wilson Pickett , James Brown,Sam and Dave, Isaac Hayes ilikuwa mwendo mdundo

4 comments:

  1. Anonymous10:39

    clarence carter dont you know this is another man's wife? Patches! hayo ndiyo yalikuwa mambo

    ReplyDelete
  2. Clarence Carter.. Too weak to fight,Getting the bills

    ReplyDelete
  3. Patrick Tsere07:34

    John na Percy Sledge je? 'When a man loves a woman'na 'Give me Your warm and tender love'. Wow wow maan. That was great brother!!Cause you get that soul feelin' maan. Hahaha

    ReplyDelete
  4. Take time to know her, Ave Maria, On the dark end of the street

    ReplyDelete

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...