YOUTUBE PLAYLIST

Tuesday, February 2, 2010


UMUHIMU WA KULIPIA MATUMIZI YA MUZIKI

Ukitunga wimbo na ukiiweka katika hali ya kushikika mara hiyo unaanza kupata haki zote za wimbo hiyo. Wimbo ni mali itokananyo na ubunifu hivyo moja kwa moja unapata haki zinazostahili kutokana na mali hiyo na ni mali yako kama vile mali nyingine. Mara wimbo utakapokuwa tayari kutumika ni muhimu kusajili katika sehemu husika ili uweze kupata ulinzi na stahili zitakazopatikana kutokana na mali hiyo. Kuna haki za aina mbili, Performance Rights na Mechanical Rights.

Performance Rights ni zile haki zitokanazo na tungo ya muziki kutumika hadharani au kurushwa hewani. Hii inajumlisha pamoja na muziki kupigwa na Live Band na, au hata muziki uliokwisha rekodiwa kupigwa hadharani katika sehemu za hadhara kama restaurants, bar, klabu za usiku, kwenye maharusi, na kadhalika. Performance rights pia ni haki zinazoambatisha muziki kurushwa hewani kupitia radio na televisheni. Kutokana na kuweko kwa haki hizi, watu binafsi na makampuni ambayo yangependa kutumia kazi hizo ni lazima wapate ruksa kwa mwenye mali na hivyo mwenye wimbo kupata royalties kila wimbo wake unaporushwa hewani au kutumika hadharani.

Mechanical Rights ni zile haki zinazohusiana na kuweka tungo katika vinasa sauti kama vile kanda CD na DVD. Hivyo mtu au kampuni inapotaka kuweka kazi ya mtu katika kinasa sauti cha aina yoyote kutalazimika kuwepo na ruksa kutoka kwa mwenye mali au taasisi ambayo ina mamalaka ya Mechanical Rights za kazi hiyo. Watunzi hupata Mechanical Rights kwa nyimbo zinaposambazwa na wauzaji.

Ili kurahisisha ufuatiliaji na uratibu wa haki zilizotajwa hapo juu copyright collecting agency au copyright collecting society hutengenezwa ambapo aidha huwa ni chombo kilichobuniwa na watunzi au chombo kilichowekwa kisheria. Chombo hiki hupewa mamlaka na wanachama pia kutoa na kusimamia leseni mbalimbali kwa kazi walizozisajiri

Kwa hapa Tanzania Bara chombo ni COSOTA na Zanzibar COSOZA. Hivi ni vyombo vilichopewa mamlaka kisheria kushughulika kwa niaba ya watunzi kufuatilia haki zao, na kukusanya mafao yatokanayo na kazi hizo.

Ujio wa vinasa sauti bora na mtandao wa intanet unawezesha mamilioni ya watu kuweza kusikiliza wimbo kwa wakati mmoja katika maeneno mbalimbali ulimwenguni. Siyo siri kuwa matumizi kama ringtones ni biashara kubwa sana ambayo wasanii hawajapata manufaa stahili kutokana na mapato ya kazi zao.

Kuweko kwa taratibu za kukusanya mirabaha kuna wapatia fulsa wanamuziki wakongwe kuendelea kupata chochote na hata kutajirika japo nyimbo zao ni za zamani, napengine haziuziki tena. Mtunzi wa wimbo wa Red red wine alikwisha kata tama kimaisha uliporekodiwa upya wimbo huo ametajirika kutokana na wimbo huo.

Kuweko kwa vinasa sauti kumepunguza umuhimu wa kuweko kwa live music, hivyo malipo ya mirabaha inawezesha wanamuziki kupata mafao yao kwa kazi zao zilizotumika badala ya wao. Ni ukweli usiopingika kuwa kuna baadhi ya shughuli haziwezi kukamilika bila ya matumizi ya muziki. Kwa mfano biashara nyingi huongezea motisha kwa kupiga muziki. Mabaa, restaurant, magari ya kusafirisha abairia, na kadhalika. Haya ni matumizi makubwa tu ya muziki.

Shughuli mbali mbali za sherehe kama vile mikutano ya kisiasa, harusi birthday party hutawaliwa na muziki ambao matumizi yake huwa hayalipiwi kinyume kabisa cha haki za kimsingi za binadamu waliotunga nyimbo zinazotumika

1 comment:

  1. Anonymous14:03

    Mimi ni mnyalukolo , je nyimbo zako umeziweka katika CD. Nilikunwa sana na wimbo "Vatige mnyakidada' ulipopigwa 96 kwenye shughuli ya kuenzi picha za kuchora za aunt Konga pale national museum. Nitaipata vipi kama ipo?

    ReplyDelete

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...