YOUTUBE PLAYLIST

Tuesday, February 2, 2010


Ujaji wa vinanda aina ya synthesizer ulitoa hukumu ya kifo kwa taaluma ya vyombo vya upulizaji katika bendi nyingi Tanzania. Msondo ngoma wamebakia na msimamo ambao umeweka Bendi hiyo katika ngazi ya pekee kutokana na kubakia na wapulizaji ambao ni wazuri sana, pichani, Mnyupe na Romario katika onyesho moja mjini Tanga

2 comments:

  1. Patrick Tsere21:48

    John kama kuna jambo ambalo Msondo wananifurahisha ni kuwa na Brand yao. Hata nyinyi Njenje you are in the same league. The two of you have established an identity katika dunia ya muziki. You deliver mduara na akina Muhidini na wenzie wanadeliver msondo. Hiyo ndiyo maana ya kuwa na brand yenu wenyewe. Nilishangaa the other time nilipoenda msondo kukuta wako vijana ambao wenye umri wa miaka 25 hadi 35 wengi haswa. Sasa kama msondo ungekuwa ni muziki uliopitwa na wakati usingekuta hao vijana. Watu wanafuata brand. Ukitaka msondo unaenda iliko na uktaka mduara unaenda iliko njenje. Njenje Oyee, Msondo Oyee

    ReplyDelete
  2. Binafsi nilisikitishwa na marudio ya nyimbo za zamani za msondo ambazo zilirejewa kwa kutumia vinanda badala ya midomo ya bata na tarumbeta.
    Lakini nawaheshimu wasanii woote wanaoendeleza zana halisi za kimuziki.
    Hii Bongo Flava..... just full of waweka sauti kuliko wasanii

    ReplyDelete

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...