YOUTUBE PLAYLIST

Thursday, February 4, 2010

Mzee Frank Humprick


Kati ya mwanamuziki ambae hajatendewa haki kutokana na kutothaminiwa kwa kazi zake ni marehemu Mzee Frank Humprick. Mzee huyu akiwa na dada zake walitunga nyimbo nyingi sana ambazo mpaka leo zinapigwa majukwaani na karibu kila bendi Afrika mashariki. Bendi nyingine zimediriki kurekodi upya nyimbo hizo tena bila hata kumtaarifu Mzee huyu au nduguze. Baya zaidi ni nyimbo zake nyingi kutambulishwa kuwa ni za Fundi Konde. Nyimbo zake kama Embe dodo imelala mchangani, Chaupele mpenzi,I am a democrat(uliopigwa marufuku wakati wa mkoloni),Kolokolola na nyingine nyingi. Mzee huyu Mtanzania aliyekuwa akiishi Lushoto mpaka kifo chake anastahili kuenziwa na wapenzi wote wa muziki Tanzania.

1 comment:

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...