YOUTUBE PLAYLIST

Tuesday, February 9, 2010

Muziki wa soul

Kila zama na vitabu vyake ni msemo unaoeleza kuhusu mambo ambayo hutokea katika kipindi fulani. Kila wakati kuna kizazi kipya, jambo ambalo kila kiza kipya kilichopo hudhani wao ndo wa kwanza. Katika miaka ya sitini kulikuwa na kizazi kipya cha wakati huo na moja ya muziki uliopendwa na kupigwa na vijana wakati huo ni muziki aina ya soul. Vijana walivaa kama wanamuziki wa soul wa wakati huo, walipiga muziki wao na bendi zilijipa majina ya bendi za soul. Ntataja baadhi ya wanamuziki ambao walipendwa na vijana wakati huo, najua kizazi kipya wa enzi hizo watakuwa na mengi ya kusema.

OTIS REDDING alileta raha kwa vibao kama Mr Pitiful, Fa-fa-fa-fa ambao Papa Wemba aliuimba tena miaka michache iliyopita. Sitting on the dock of the Bay, Respect, na wimbo ambao kila bendi ya soul iliupiga Direct Me. Otis alifariki katika ajali ya ndege ya kukodi na wanamuziki wenzake wane wa kundi lake la Barkays


Wilson Pickett alizaliwa March 18 1941, na kufariki kwa ugonjwa wa moyo Alhamisi 19 January 2006 alipendwa na nyimbo zake kama In the Midnight Hour, Don’t Fight It, Ninety-Nine and a Half (Won’t Do), She’s So Good to Me, Land of a 1,000 Dances,
Mustang Sally, na Funky Broadway nakuigwa sana na bendi za vijana wakati ule

James Brown huyu alikuwa ni mzee wao, alipewa majina mbalimbali kama Soul Brother Number One, the Godfather of Soul, the Hardest Working Man in Show Business, Mr. Dynamite, the Original Disco Man. Na mzee huyu ndo alikuwa kinara wa soul music miaka ya sitini, alikuwa mwanzilishi wa funk katika miaka ya 70, na alitoa mchango katika rap music miaka ya themanini. Pia alijua kucheza, Michael Jackson alikiri kuwa ile moonwalk aliipata toka kwa James Brown. JB alikuwa na nyimbo nyingi sana nitaje chache tu, The Popcorn, Mother Popcorn, Papas got a brand new bag, I am black and proud, Sex machine, James alifariki 25 Disemba 2006. Muhimu kutaja kundi lake the Famous Flames aliloanza nalo toka 1955.

Clarence Carter mwimbaji kipofu ambaye aliwakamata vijana kwa nyimbo kama too weak to fight, getting the bills ,slip away, patches

Aretha Franklin- mwanamke wa shoka huyu alipendwa sana kwa nyimbo zake kama respect, save me na think,

No comments:

Post a Comment

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...