YOUTUBE PLAYLIST

Tuesday, February 16, 2010

Kwa heri Juma Mwendapole

Kwa masikitiko makubwa nimepata taarifa ya kifo cha mdau muhimu wa muziki wa dansi Juma Mwendapole. Amefariki Ijumaa tarehe 12 February 2010 na kuzikwa kesho yake. Mwendapole ndiye aliyekuwa mmiliki wa Bendi ya Afriso Ngoma iliyokuwa na wanamuziki maarufu kama Lovy Longomba. Kwa miaka ya karibuni wanamuziki wengi wamekuwa wakimtegemea kwa kukodi vyombo vya muziki toka kwake. Bendi nyingi zisingekuweko kama si msaada wa Juma Mwendapole.
Mungu Amlaze pema peponi Amin

9 comments:

  1. Danielle23:26

    Please can you tell me if this is Baba-Issa of Msasani district?

    ReplyDelete
  2. Unfortunately I have to say Yes. Pole sana

    ReplyDelete
  3. Uncle John.
    Naomba unikumbushe / unisaidie kuweka kumbukumbu sawa. Afriso Ngoma ndiko alikoibukia Ally Choki ama Eddy Sheggy? Ni bendi hii iliyoimba Milima ya kwetu? Najaribu kuweka picha sawasawa lakini naona nahitaji msaada wako.
    Asante

    ReplyDelete
  4. R.I.P Juma Mwendapole!

    ReplyDelete
  5. Hapana Choky aliibukia Bantu kwa Hamza Kalala, bendi iliyoimba Milima Ya Kwetu ilikuwa ni Super Rainbow,bendi ya Mwananyamala, waimbaji wakiwa Eddy Sheggy na Emma Mkelo

    ReplyDelete
  6. Danielle23:28

    Ndiyo pole sana :( I lived at their home in 2007 and they treated me like family. Please send my sympathy to mama, Issa, Saidi and my little toto Salima.

    ReplyDelete
  7. Asante saana Uncle
    Naendelea kujifunza na kuboresha kumbukumbu zangu.

    ReplyDelete
  8. Anonymous11:52

    KWANZA NATOA POLE KWA FAMILIA YA MWENDAPOLE KWA MSIBA,MOLA AILAZE ROHO YAKE PEPONI.

    DEKULA KAHANGA SWEDEN

    ReplyDelete
  9. Anonymous18:20

    pole kwa familia na wadau wa muziki hapa africa na ulimwenguni kote tuko pamoja kaka Kitime naamini kwa pamoja tunaweza kufikisha ujumbe na kutangaza muzkiki wetu mbali zaidi

    ReplyDelete

SAFARI ZANGU NA BENDI sehemu ya kwanza.

  TANCUT ALMASI ORCHESTRA  wakiwa Jamhuri Stadium Dodoma   Sikumbuki ni safari ngapi za kimuziki nilizowahi kuzifanya hapa nchini katika m...